Mabingwa wa
kihistoria nchini Ujerumani, Bayern Munich watakuwa tayari kumuuza kiungo wao
mwenye uzoefu mkubwa na nahodha wa timu ya taifa ya Ujerumani, Bastian Schweinsteiger kama tu kiungo huyo atahitaji
kuondoka.
Bastian
mwenye umri wa miaka 31 hivi sasa amekuwa akihusishwa na kuihama klabu hiyo
tangu kutua kwa kocha Mhispania Pep Guardiola.
Manchester
United wameripotiwa mara kadhaa kuhitaji saini ya kiungo huyo ambaye aliwahi kufanya
kazi kwa mafanikio makubwa na kocha wa sasa wa Manchester United, Louis Van
Gaal.
Nafasi ya
kiungo huyo inaonekana mashakani katika kikosi hicho cha Pep Guardiola kutokana
na uwepo wa kiungo Thiago Alcantara ambaye ni kipenzi cha Guadiola huku
akionekana kuuweza mfumo wa tik-taka unaofundishwa na kocha huyo.
Aidha Xabi
Alonso naye anafanya umuhimu wa mchezaji huyo kupungua.
Lakini
mkurugenzi Mtendaji wa klabu hiyo ya Bayern Munich, Karl-Heinz Rummenigge
amesema kiungo huyo hajaonesha dalili zozote za kutaka kuondoka.
0 comments:
Post a Comment