Thursday, May 28, 2015

Vijana wakiandaliwa kuwa mastaa wa badaye, lakini mazingira wanayoandaliwa ni bonge la tatizo

Timu ya vijana wenye umri wa chini ya miaka 12 Jinu Star ya Mtoni Mtongani, Manispaa ya Temeke imeomba kusaidiwa vifaa vya michezo ili iweze kusonga mbele katika juhudi zake za kuinua soka la vijana nchini ambao watakuja kucheza kwenye ngazi za vilabu na timu ya Taifa ‘Taifa Stars’ muda mfupi ujao.

Kocha wa timu hiyo Charles Beka amesema, timu hiyo ina upungufu wa vifaa vya michezo ikiwemo mipira, viatu pamoja na jezi mbavyo ndio changamoto kubwa kwenye timu hiyo.


“Mimi unavyoniona hapa ndio kocha wa timu hii, katibu, mwenyekiti na kila kitu hapa, sina msaidizi na mimi ndiyo nashughulika na kilakitu kwenye timu hii. Kwenye timu yetu tunashindwa kufanya mambo mengi ili kufikia malengo kwasababu ya upungufu wa vifaa”, amesema Beka.

“Mipira tuliyonayo ni mitano tu, tena mibovu lakini ndiyo tunaitumia hiyohiyo kwenye mazoezi kitu ambacho kinatupa wakati mgumu. Wakati tunajifunza ufundi wa mpira (kuchezea mpira) tunahitaji angalau mpira mmoja utumiwe na wachezaji wawili japo kiuhalisia inatakiwa kila mchezaji awe na mpira wake”, ameongeza Beka.

“Changamoto nyingine ni ushirikiano duni toka kwa wazazi japo sio wote, baadhi ya wazazi wamekuwa wakiwazuia watoto wao kuja kufanya mazoezi lakini wakati mwingine tumekuwa tukiwaomba michango kwa ajili ya kutengenezea mipira inapoharibika au pesa ya nauli tunapohitaji kusafiri kwenda kucheza mechi za kirafiki, wazazi wengine wamekuwa wagumu kujitolea. Timu haina mdhamini kwahiyo tunapata changamoto kubwa”, Beka alisisitiza.

Kocha huyo wa kujitolea ametoa wito kwa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) kuangalia timu za mtaani ambazo zinafundisha soka kwa vijana ili kushirikiana kwa pamoja katika kutatua changamoto zinazowakabili na kuwajumuisha wachezaji wenye vipaji kwenye timu za Taifa za vijana.

0 comments:

 
https://www.sexmutant.com/ https://www.sexindrag.com/ porn movies sex videos hd porno video