Tuesday, May 5, 2015

Mechi ya kwanza uwanja wa Taifa, Yanga na Ndanda fc zilitoka suluhu pacha ya bila kufungana.

YANGA SC wamepigwa mkwara na Ndanda fc wenye uchu wa kuvuna pointi tatu za mwisho na kubakia ligi kuu.
Mpaka sasa Ndanda fc wapo kwenye hatari ya kushuka daraja wakijikusanyia pointi 28 katika nafasi ya 11, sawa na Tanzania Prisons, Mgambo JKT, Stand United wenye idadi ya pointi hizo na timu zote zimebakiwa na mchezo mmoja tu kumaliza msimu huu mgumu wa ligi kuu.
Kocha mkuu wa Ndanda fc, Meja Mstaafu, Abdul Mingange amesema wamejiandaa vilivyo kupambana na Yanga mei 9 mwaka huu uwanja wa Nangwanda Sijaona, Mtwara na kuvuna pointi tatu muhimu.
“Sisi tutapambana mpaka tone la mwisho, Yanga ni timu bora na Mabingwa, lakini kwenye mpira lolote linaweza kutokea. Waje wakijua Ndanda inaska pointi tatu na imejipanga kuzipata”. Amesema Mingange na kuongeza: “Tunalingana pointi na timu tatu katika msimamo (pointi 28), hapo kila mtu anaweza kushuka daraja, tunafahamu ugumu wa mechi ya jumamosi, lakini tuko tayari nakwambia!”.

0 comments:

 
https://www.sexmutant.com/ https://www.sexindrag.com/ porn movies sex videos hd porno video