Tuesday, May 5, 2015

KIMAHESABU watu wengi wameshaishusha daraja Polisi Morogoro msimu huu kutokana na kuwa na pointi 25 tu katika msimamo baada ya kucheza mechi 25.
Mechi ya mwisho mei 9 mwaka huu, Polisi watachuana na Mbeya City katika uwanja wa Sokoine Mbeya na mechi hiyo itaamua hatima ya Maafande hao wanaopumulia mashine.
Lakini kuna kitu kinasahaulika ambacho ni tofauti ya magoli ya kufunga na kufungwa.
Mpaka sasa Polisi wapo mkiani wakiwa wamefunga magoli 16 na kufungwa 26, tofauti ya magoli ni -10.
Stand United wenye pointi 28 katika nafasi ya 13 wamefunga magoli 22 na kufungwa 34, tofauti ya magoli ya kufunga na kufungwa ni -12.
Mgambo JKT waliopo katika nafasi ya 12 na pointi 28  wamefunga magoli 18 na kufungwa 28, tofauti ya magoli ya kufunga ni -10 sawa na Polisi Morogoro.
Maana yake kama Mgambo watafungwa na Azam fc 1-0 mei 9 mwaka huu, Polisi akashinda 1-0 dhidi ya Mbeya City atakuwa na magoli 17 ya kufunga na 26 ya kufungwa, tofauti itakuwa -9 na watawazidi Mgambo watakaokuwa na wastani wa -11. Maana yake Mgambo watashuka daraja kwasababu Polisi watafikisha pointi 28, na Mgambo 28, lakini Polisi watakuwa juu kwa tofauti ya magoli.
Kama Stand watafungwa na Ruvu Shooting mei 9 mwaka huu watakuwa na magoli 12 ya kufungwa na 35 ya kufungwa, tofauti itakuwa -13. Kwa maana hiyo Stand na Mgambo watakuwa chini ya Polisi kama wataifunga Mbeya City.
Ndanda fc wana pointi 28 mpaka sasa katika nafasi ya 12. Wamefunga magoli 20 na kufungwa magoli 29, tofauti ni -9. Endapo watapata sare siku ya mwisho dhidi ya Yanga, matokeo mengine yakatokea kama nilivyoeleza hapo juu, maana yake Mgambo JKT na Stand United watakuwa wameshuka daraja.
Tanzania Prisons wamebakiza mechi moja dhidi ya Kagera Sugar, lakini kwasasa wapo nafasi ya 10 kwa pointi zao 28. Kitu kizuri ni kwamba wamefunga magoli 18 na kufungwa 22, tofauti ni -4. Huu ni wastani mzuri ukilinganisha na timu za chini yake.
Kama atafungwa 1-0, atakuwa amefunga magoki 18 na kufungwa 23, tofauti itakuwa -5. Wastani ambao utamsaidia kama matokeo mengine yatatokea kama nilivyoeleza hapo juu.
Kwa mahesabu hayo, bado Polisi Morogoro hawajashuka daraja, cha msingi washinde mechi ya mwisho, halafu wasikilizie kwingine kutakuwa na matokeo ya aina gani. Huu ni mpira wa miguu, matokeo mpaka dakika 90’ zikamilike.

0 comments:

 
https://www.sexmutant.com/ https://www.sexindrag.com/ porn movies sex videos hd porno video