Tuesday, May 5, 2015

RAMADHAN Singano ‘Messi’ aliifungia Simba goli moja katika ushindi wa 2-1 dhidi ya Azam fc katika mechi ya ligi kuu soka Tanzania bara iliyopigwa mwishoni mwa juma lililopita uwanja wa Taifa.
Goli lingine likifungwa na Ibrahim Hajib, huku bao la kufutia machozi la Azam likifungwa na Mudathir Yahya.
Wakati wa kushangilia goli lake, Singano alivua jezi na kuonesha fulana yake iliyoandikwa kwa maneno ya kiarabu yenye maana ya ‘Fadhila au neema za Mwenye enzi Mungu zipo juu yangu’, Kwa mujibu wa mtaalamu mmoja wa lugha ya kiaarabu aliyezungumza na MPENJA BLOG.
Alipofuatwa Singano mwenyewe alisema: “Mungu ndio kila kitu kwangu, mimi ni Muislamu, naiheshimu dini yangu na mwenye enzi Mungu ndiye kila kitu kwangu, fadhila zake ni kubwa kwangu ndio maana nimeendelea kucheza kwa mafanikio ndani ya klabu yangu ya Simba”.
Singano ambaye ni muumini mzuri wa dini ya kiislamu na wenzake wanamuita ‘ustadhi’ amefunga magoli matano msimu huu na amekuwa kwenye kiwango bora kwa muda mrefu sasa.

Kuhusu ndoto za soka Singano anesema: “Nina malengo ya kufika mbali kama Mungu akipenda, najituma na kuyalinda mazoezi na kiwango changu, ipo siku milango itafunguka”.

0 comments:

 
https://www.sexmutant.com/ https://www.sexindrag.com/ porn movies sex videos hd porno video