
Kocha wa Chelsea Jose Mourinho hajashinda hata mara moja tuzo ya kocha bora wa mwezi msimu huu, hali hiyo inamfanya kuwa kocha wa kwanza kuchukua ndoo bila ya kutwaa tuzo hiyo tangu.......Jose Mourinho.
Kocha huyo Mreno alizungumza suala la timu yake kufanyiwa njama na baadhi ya viongozi wa ligi hiyo na kutangazwa kwa kocha wa Leicester Nigel Pearson kuwa kocha bora wa mwezi Aprili kumuongeza uzito juu ya madai yake.
Katika historia ya ligi kuu nchini Uingereza, kumekuwa na matukio mawili tu ya kocha ambaye timu yake imetwaa ubingwa wa ligi halafu hajawahi kuchukua tuzo ya kocha bora wa mwezi hata mara moja kwa msimu mzima, ambapo mara ya kwanza kutokea ilikuwa ni msimu wa 2005-06, wakati Mourinho alipoipa ubingwa Chelsea na kujirudia tena mwaka huu, ambapo kwa mara nyingine tena Mourinho amefanya hivyo.

Hii ni mara ya pili kwa Mourinho kutwaa ubingwa bila kuwa kocha bora wa hata mwezi mmoja.

Kocha wa Leicester Nigel Pearson ametwaa tuzo ya kocha bora wa mwezi Aprili, hii inamaanisha Mourinho kwa mara nyingine tena hatotwaa tuzo hii

Mourinho ni kocha pekee ambaye ameipa timu ubingwa bila kutwaa tuzo ya kocha bora mwezi hata mara moja kwa msimu mzima.
Ikiangaliwa katika misimu iliopita, ianonesha kuwa kocha wa zamani wa Man United Sir Alex Ferguson alitwa(2002-03) na Arsene Wenger (2001-02) walichukua tuzo hizo mwezi Aprili kama makocha wenye mafaniko msimu mzima.
Mourinho anaweza kutajwa kama kocha wa msimu katika EPL baadaye msimu ukimalizika mwezi mei, lakini hiyo bado haitoondoa maswali mengi juu ya maamuzi hayo kwa Chelsea.



| MONTH | 2004-05 | 2005-06 | 2006-07 | 2007-08 | 2013-14 | 2014-15 |
|---|---|---|---|---|---|---|
| August | Arsene Wenger (Arsenal) | Stuart Pearce (Manchester City) | Sir Alex Ferguson (Manchester United) | Sven-Goran Eriksson (Manchester City) | Brendan Rodgers (Liverpool) | Garry Monk (Swansea) |
| September | David Moyes (Everton) | Paul Jewell (Wigan) | Steve Coppell (Reading) | Arsene Wenger (Arsenal) | Arsene Wenger (Arsenal) | Ronald Koeman (Southampton) |
| October | Harry Redknapp (Portsmouth) | Paul Jewell (Wigan) | Sir Alex Ferguson (Manchester United) | Mauricio Pochettino (Tottenham) | Sam Allardyce (West Ham) | |
| November | Jose Mourinho (Chelsea) | Rafael Benitez (Liverpool) | Steve Coppell (Reading) | Alan Pardew (Newcastle) | Alan Pardew (Newcastle) | |
| December | Martin Jol (Tottenham) | Rafael Benitez (Liverpool) | Sam Allardyce (Bolton) | Manuel Pellegrini (Manchester City) | Manuel Pellegrini (Manchester City) | |
| January | Jose Mourinho (Chelsea) | David Moyes (Everton) | Rafael Benitez (Liverpool) | Manuel Pellegrini (Manchester City) | Ronald Koeman (Southampton) | |
| February | Sir Alex Ferguson (Manchester United) | Alan Pardew (West Ham) | Sir Alex Ferguson (Manchester United) | Sam Allardyce (West Ham) | Tony Pulis (West Brom) | |
| March | Harry Redknapp (Portsmouth | Sir Alex Ferguson (Manchester United) | Jose Mourinho (Chelsea) | Brendan Rodgers (Liverpool) | Arsene Wenger (Arsenal) | |
| April | Stuart Pearce (Manchester City) | Harry Redknapp (Southampton) | Martin O'Neil (Aston Villa) | Tony Pulis (Crystal Palace) | Nigel Pearson (Leicester) |
Mara kadhaa Mourinho amekuwa akikosolewa sana kwa kutumia mbinu ambazo watu wengi hawafurahishwi nazo, Japokuwa ukweli ni kwamba ni Manchester City pekee ndio wamewazidi Chelsea kwa magoli mpaka sasa.
Ni wachache tu wanaoweza kukataa mafanikio aliyoyapata tangu arudi kwa mara nyingine tena EPL.
Amefanikiwa kuendana na sheria ya UEFA ya matumizi ya fedha (Uefa's Financial Fair Play) ambapo Mourinho ameipata ubingwa Chelsea huku akiwa pia ametengeneza faida ya kutosha klabuni hapo, kitu ambacho hakijafanyika kwa takribani miaka nane klabuni hapo.
Wametangazwa mabingwa huku wakiwa na michezo mitatu mkononi na wanaongoza kwa pointi 13 zaidi ya timu inayoshika nafasi ya pili.
ClearlyKwa ufasaha kabisa ,lakini hata hivyo jopo la wapiga kura lenye watu zaidi ya 40 halijavutiwa na hilo.
Mwanzoni mwa msimu, alipoulizwa juu ya hilo, Mourinho alisema.




'Mimi sijali,' ' Lakini kuna kitu ambacho hakipo sawa kwa sababu, kwa miaka minne ambayo nimekaa hapa,nimeshinda tuzo hii mara tatu tu.
'Hivyo, Kiukweli, niseme tu hawanipendi. Lakini sijali hilo mimi. Ninachotaka ni timu yangu kushinda tu mimi.'
Mwezi Disemba, mtoaji waa tuzo hiyo Andrew McDougall alikataa kabisa kuwa hakuna watu wasiompenda Mourinho katika majadiliano yao.
Alisema: 'Jopo linaundwa na takribani watu 40 ,wote ni watu wa mpira, kuna wachezaji wa zamani, waandishi wa masuala ya mpira na wawakilishi kutoka chama cha makocha wa ligi kuu, FA yenyewe na bodi ya ligi





'Mtu nayeshinda ndio mtu anyepata kura nyingi sana . Nina uhakika kabisa uwa jina la Jose mata zote huwa linakuwepo, lakini huwa anazidiwa. Chukua tu mfano mdogo, Sam Allardyce alishinda mwzi Octoba, akiwa ameipa timu yake ushindi mara 3 na sare moja.
'Mzani kati yake na Jose uliwekwa, lakini Mourinho ukiangalia ana kikosi bora, huo ndio ukweli halisi na hakuna upendeleo wowote.'
MAKOCHA WA LIGI KUU NCHINI UINGEREZA WALIOWAHI KUSHINDA TUZO YA KOCHA BORA WA MWEZI
A look at Premier League winning managers and how many Manager of the Month awards they took on the way to the title:
93-94 Manchester United (Sir Alex Ferguson 1); 94-95 Blackburn Rovers (Kenny Dalglish 1)
95-96 Manchester United (Sir Alex Ferguson 2); 96-97 Manchester United (Sir Alex Ferguson 1)
97-98 Arsenal (Arsene Wenger 2) 98-99 Manchester United (Sir Alex Ferguson 2)
99-00 Manchester United (Sir Alex Ferguson 3) 00-01 Manchester United (Sir Alex Ferguson 1)
01-02 Arsenal (Arsene Wenger 1 ); 02-03 Manchester United (Sir Alex Ferguson)
03-04 Arsenal (Arsene Wenger 2); 04-05 Chelsea (Jose Mourinho 2);
05-06 Chelsea (Jose Mourinho 0); 06-07 Manchester United (Sir Alex Ferguson 3);
07-08 Manchester United (Sir Alex Ferguson 2); 08-09 Manchester United (Sir Alex Ferguson 2)
09-10 Chelsea (Carlo Ancelotti 1); 10-11 Manchester United (Sir Alex Ferguson 1);
11-12 Manchester City (Roberto Mancini 1); 12-13 Manchester United (Sir Alex Ferguson 1)
13-14 Manchester City (Manuel Pellegrini 2) 14-15 Chelsea (Jose Mourinho 0)


0 comments:
Post a Comment