Tuesday, May 5, 2015


 Mwenyekiti wa kamati ya usajili ya Simba, Zacharia Hans Poppe


UTANI wa jadi una raha yake! Hivyo ndivyo unavyoweza kusema! Ile ishu ya Simba kuishangilia Yanga katika mechi ya kesho dhidi ya Azam  fc imekuwa tamu ambapo kila upande unasema yake.
Kama Yanga wataifunga Azam fc kesho itakuwa nafuu kwa Simba wanaoiwania nafasi ya pili kwa udi na uvumba.
Azam akipoteza mchezo wa kesho na kutoka sare  mechi ya mwisho mei 9 mwaka huu dhidi ya Mgambo JKT, halafu Simba ikashinda mechi yake ya mwisho dhidi ya JKT Ruvu, basi Mnyama atachukua nafasi ya pili.
Katika msimamo Azam wanashika nafasi ya pili kwa pointi 45 baada ya kucheza mechi 24, wakati Simba wanashika nafasi ya tatu wakijikusanyia pointi 44 kwa kucheza mechi 25.
Turudi kwenye utani wa jadi! Leo mkuu wa Idara ya habari na mawasiliano wa Yanga, Jerry Muro amesema: “Kama wao (Simba) wataona kuna haja ya kuishabikia Yanga waje, wavae jezi za Yanga wakiongozwa na viongozi wao, wachezaji watapata morali,  wataweza kushinda. Wao waite matawi yao, wavae jezi za Yanga, wachezaji wapate morali. Akina Msuva wakiona makofi yamekuwa mengi wataongeza mbwembwe na kufunga, niwaombe viongozi wa Simba wavae jezi za Yanga waje kuishangilia Yanga, vijana wa Yanga watahamasika wakimuona Hans Poppe amevaa jezi ya Yanga, yuko mbele na kitambi anashangilia Yanga au Aveva (Evans-Rais wa Simba) anashangilia Msuva funga..funga.. wanaweza kushinda”.

Baada ya maneno hayo ya Muro, mwenyekiti wa kamati ya usajili ya Simba, Zacharia Hans Poppe amejibu mapigo kwa kusema: “Sijui nani anaweza kuwapigia magoti hao Yanga, mimi ninachoweza kusema uwezo wetu ndio umetufikisha hapa, watu wengine wasiwe na cha kutafuta, kama yatatokea matokeo yoyote wakawafunga basi yatokee hivyo lakini sio kwa kuwabeba. Kama mechi zetu za nyuma hatukucheza vizuri, basi ni matatizo yetu, tumeyakoroga wenyewe, msimu ujao unakuja, tutafanya vizuri na tutachukua nafasi nzuri, lakini hatuwezi kuwaomba Yanga, mimi binafsi sitaweza kwenda kuwaomba, wala sina haja ya kufanya hivyo, sisi tutaingia kwenye mashindano, tutashinda kwa uwezo wetu na tukifungwa tutafungwa kwa uwezo wetu”.

0 comments:

 
https://www.sexmutant.com/ https://www.sexindrag.com/ porn movies sex videos hd porno video