Thursday, April 30, 2015

NDANDA FC wametangaza vita kuelekea mechi zao mbili za mwisho dhidi ya Kagera Sugar na Dar Young Africans.
Kesho kutwa Ndanda watachuana na Kagera Sugar uwanja wa Nangwanga Sijaona na mei 9 mwaka huu katika uwanja huo huo watakabiliana na mabingwa Yanga kufunga msimu wa 2014/2015.
Mpaka sasa Ndanda inashika mkia katika msimamo ikiwa na pointi 25 baada ya kucheza mechi 24, sawa na Prisons wenye pointi 25 nafasi ya 12 wakicheza mechi 24, pia Polisi Moro wapo nafasi ya 13 kwa pointi 25 kufuatia kushuka dimbani mara 25.
Kuelekea mechi ya jumamosi ambayo Ndanda lazima washinde kama wanataka kubaki ligi kuu, afisa habari wa klabu hiyo, Idrissa Bandali amesema kila mechi ya ligi kuu ni ngumu na wamejipanga kuvuna pointi sita zilizobaki.
“Kila mechi ya ligi kuu ni ngumu, mechi ya Kagera sio rahisi, lakini inategemea na maandalizi yako, tutaingia kwenye mechi zote tukihitaji ushindi kuanzia ya Kagera na baadaye ya Yanga.” Amesema Bandali na kuongeza: “Unajua mpira wa miguu ni mchezo wa dakika 90’, pia kusema timu imeshuka msimu huu ni mpaka pale mechi za mwisho zitakapokamilika  mei 9 mwaka huu. Hapo tutajua kama tunashuka au tunabaki”.
Bandali ameongoza kuwa tayari bingwa ameshajulikana, lakini nani anashuka ni mpaka tarehe 9.

“Tunataka kuondoa fikra za watu kuwa tunashuka, hatuwezi kuondoa kwa maneno bali ni kwa ushindi, tunaingia uwanjani tukiwa na changamoto kubwa, lakini tutafanya kwa vitendo”.

0 comments:

 
https://www.sexmutant.com/ https://www.sexindrag.com/ porn movies sex videos hd porno video