Thursday, April 30, 2015

NAHODHA wa Simba, Hassan Suleiman Isihaka anaumwa maralia na Typhoid na amesisima kufanya mazoezi madogo madogo aliyoanza kwa ajili ya kuimarisha mguu wake.

Isihaka akiwa na daktari wa Simba, Yassin Gembe siku aliyoumia

Beki huyo mstaarabu aliyeumia aprili 18 mwaka huu Simba ikifa 2-0 dhidi ya Mbeya City katika uwanja wa Sokoine na kutolewa nje dakika ya 23’, ameiambia MPENJA BLOG kuwa ameshapima Hospitali na sasa yupo kwenye dozi.

“Ninasumbuliwa na maralia na typhoid, ilinianza jumamosi baada ya mechi dhidi ya Ndanda fc, nimeenda Hospitali na kupatiwa dawa”. Isihaka ameuambia mtandaon huu na kuongeza:“Mguu unatengamaa fresh, lakini tatizo ni malaria, nilishaanza mazoezi madogo madogo, lakini sahizi naumwa”

Mlinzi huyo kipenzi cha kocha wa Simba, Goran Kopunovic amewatakia kila la kheri wachezaji wenzake kuelekea mechi ya mwishoni mwa juma hili.

“Mimi niwatakiwa kheri wachezaji wenzangu kwenye mechi ya jumapili dhidi ya Azam fc, naamini watacheza vizuri na kushinda ‘inshaallah’”

Isihaka toka aumie amekosa mechi mbili dhidi ya Mgambo JKT waliyoshinda 4-0 na ile ya Ndanda fc ambayo Simba waliibuka kidedea kwa magoli 3-0.


Kutokana na kukosekana kwa Isihaka, Kopunovic anawatumia walinzi wawili wa kati kutoka Uganda, Juuko Mursheed na Joseph Owino.

0 comments:

 
https://www.sexmutant.com/ https://www.sexindrag.com/ porn movies sex videos hd porno video