Thursday, April 30, 2015

Chidiebele mwenye jezi namba 9 kwenye bukuta 

MNIGERIA anayekipiga ‘chama la wana’ Stand United, Abasalim Chidiebele amekiri kukumbana na changamoto kubwa kutoka kwa mabeki wa timu za ligi kuu soka Tanzania bara.

Chidiebele ambaye ameifungia Stand United magoli 9 mpaka sasa ameiambia MPENJA BLOG kuwa walinzi wa timu za ligi kuu wanajua kuwa yeye ndiye mshambuliaji tishio katika timu yake, hivyo wanamkaba ipasavyo kuhakikisha hawadhuru.

“Walinzi wa timu pinzani wanajua kuwa Chidiebele (Abasalim) ni mtu hatari Stand United, wananikaba na kuninyima nafasi ya kufunga, kila mechi mabeki wananiangalia sana” Amesema Chidiebele na kusisitiza kuwa “Mimi ni mshambuliaji, natafuta janja zangu na kuwaadhibu, najua huu ni mchezo wa kulipwa. Sahizi nafanya juhudi ya kuisaidia timu yangu kubaki ligi kuu, haya ndiyo malengo yangu makubwa”.

Stand United ipo kwasasa ipo nafasi ya 11 ikijikusanyia pointi 28 katika mechi 24 walizocheza.


Timu hiyo ya wapigadebe wa Shinyanga mjini imebakiza mechi dhidi ya Coastal Union uwanja wa Mkwakwani tangu itayochezwa jumapili hii na mechi ya mwisho ni mei 9 mwaka huu watapochuana na Ruvu Shooting uwanja wa nyumbani wa CCM Kambarage Shinyanga.

0 comments:

 
https://www.sexmutant.com/ https://www.sexindrag.com/ porn movies sex videos hd porno video