Thursday, April 30, 2015

YANGA SC wameondoka usiku wa jana kwenda nchini Tunisia kupitia Dubai kuwafuata wapinzani wao  Etoile du Sahel.

Etoile na Yanga zitachuana keshokutwa katika mechi ya marudiano ya hatua ya 16 bora ya kombe la shirikisho  baada ya kutoka sare ya 1-1 mchezo wa kwanza uliopigwa uwanja wa Taifa Dar es salaam takribani wiki mbili zilizopita.

Yanga wanahitaji ushindi au sare ya kuanzia magoli 2-2 ili kusonga mbele moja kwa moja.

MPENJA BLOG ilikuwepo uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Mwalimu Julius Nyerere jijini Dar es salaam wakati Yanga wanakwea ‘pipa’ na ulipata nafasi ya kuzungumza na kocha Hans van der Pluijm.

“Hatuna cha kupoteza kwenye mchezo huo, tulitoka sare ya kufungana goli 1-1 tukiwa nyumbani hivyo tunahitaji kupata ushindi au sare ya magoli kuanzia mawili ili tuweze kusonga mbele. Tumejipanga vizuri kwa hili na wachezaji wote tunaokwenda nao wanatambua umuhimu wa mchezo huo”, alisema Pluijm na kusisitiza: “Etoile ni timu nzuri na ina uzoefu mkubwa kwenye michuano ya Afrika na kila mtu aliona aina ya soka walilocheza hapa, tunawaheshimu na tumejipanga ili kukabiliana nao na kuibuka na ushindi kwenye mchezo huo.

 “Ni lazima tucheze soka la kushambulia na kupata magoli ya mapema lakini wakati huohuo tunatakiwa kuwa makini sana kuhakikisha haturuhusu kufungwa goli, nimezungumza na wachezaji na kila mtu anajua majukumu yake. Najua kwenye soka lolote linaweza kutokea na tukasonga mbele kwa hatua inayofuata”.

Ukiyasoma maneno hayo ya Pluijm kuna mambo matatu anayochukulia uzito wa hali ya juu;

Mosi, kujiamini ndio silaha ya mafanikio; Pluijm anaposema hawana cha kupoteza zaidi ya kutafuta ushindi ugenini tena wa magoli mengi ni ishara ya yeye mwenye kujiamini na kwa maana hiyo hata wachezaji wake wamejiamini.

Wataalamu wa mpira wanasema wachezaji wanacheza kuakisi falsafa ya mwalimu, kama mwalimu atahofia mechi na kuonesha hofu yake kwa wachezaji basi na wao watahofia. Kocha akijiamini hata wachezaji watajiamini pia. Pluijm ameonesha kujiamini zaidi na hana shaka na mechi hiyo.

Pili; Pluijm anafahamu ubora wa wapinzani wao, yeye ni kocha, aliwaona mechi ya kwanza na kubaini wana uzoefu mkubwa na muunganiko wa timu, kwa maana hiyo ataingia uwanjani kwa tahadhari kubwa akijua anacheza na timu bora.

Tatu; anajua faida ya kutofungwa mapema, kushambulia na kikubwa zaidi ni kucheza kwa nidhamu kwa lengo la kujilinda. Makocha wengi wanakosea katika mipango ya mechi, anawahamasisha wachezaji kushambulia kwasababu anahitaji matokeo, lakini anashindwa kuwakumbusha kwa haraka wachezaji wake kuhusu nidhamu ya ulinzi. Pluijm anasema watashambulia na kujilinda kwa nidhamu ya hali ya juu, hilo ni jambo muhimu.

Lakini mbali na hayo, Mtandao huu unaheshimu uwezo wa mabingwa wa Tanzania,  Dar Young Africans, wanaweza kushinda, kutoa sare au kufungwa kutokana na kikosi chao kuwa na wachezaji wenye uwezo binafsi na kimekaa kwa pamoja angalau kwa muda mrefu.

Amissi Tambwe, Mrisho Ngassa, Simon Msuva ni wachezaji wanaoweza kuamua matokeo kwa kutegememea ubora wa Haruna Niyonzima na Salum Telela dimba la kati.

Etoile du Sahel ni timu bora barani Afrika, ina wachezaji wazuri kwa kuangalia kipaji cha mchezaji mmoja mmoja bila kusahau muunganiko wa timu ‘Team Chemistry’.

Wanaweza kujilinda, kudhibiti kiungo cha mpinzani, kupiga pasi za kupenyeza, kutengeneza mashambulizi na kumalizia kazi yao kwa ustadi mkubwa.

Kutokana na ubora wao na uzoefu wao katika soka la kimataifa kunafanya watu wengi wawadharau Yanga na kuona wanaenda kufa nyingi Tunisia. Kimajina, hakuna ushindani baina ya timu hizi, Etoile ni timu kubwa yenye mafanikio kuliko Yanga kwa ngazi ya kimataifa, lakini lazima ukumbuke kuwa huu ni mpira, chochote kinaweza kutokea.

Inatokea mara nyingi timu bora inapoteza, mpira wa miguu ni mchezo wa makosa, unaweza kuongoza kwa kila kitu, umiliki wa mpira, mashuti yaliyolenga lango, mashuti ambayo hayakulenga lango, kona nyingi, lakini ukafungwa goli moja tena la kukuotea tu na mwisho ukapoteza mechi.

Yanga wanaweza kushinda wakijiamini, lazima watashambuliwa sana, lakini ni kawaida katika soka hususani unapokuwa ugenini, cha msingi ni kuwa na nidhamu ya ulinzi na kujitahidi kuua viungo wa Etoile wasisambaze mipira kwa viungo wao washambuliaji na washambuliaji wa kati.

Timu za uarabuni ni maarufu sana kwa mipango ya nje na ndani ya uwanja, wanajua namna ya kumtoa mpinzani mchezoni, wanajua namna ya kucheza na waamuzi.

Unaweza kutua uwanja wa Ndege ukakalishwa saa nne bila kumuona mwenyeji wako halafu baadaye ukaletewa basi bovu, ukanyimwa uwanja mzuri wa  mazoezi, lengo ni kukufanya uathirike kisaikolojia.

Wanajua wazi kuwa mchezaji anaweza kuwa na ufundi, mbinu, utimamu wa mwili, lakini akiwa hovyo kisaikolojia anafanya vibaya.

‘Uchawi’ pekee wa Yanga kushinda ni kutegemea kufanyiwa‘fitina’, lakini ‘wasipaniki’ wajue uarabuni ni mahala pa fitina. Unajua ukijitayarisha kwa jambo baya unalokwenda kufanyiwa na mpinzani wako na kujiandaa kupamabana nalo kama changamoto ya kawaida, unaifanya akili iwe sawasawa. Cha msingi wajiandae kisaikolojia kupambana nao, wawapotezee kwa mambo yao mabaya, wachukulie  ni changamoto tu.

 Viongozi, makocha, wachezaji waelekeze nguvu kwenye mchezo, wasifirikie fitina, wasikae kiunyonge hotelini na wachezaji, wasiwahusishe wachezaji kwa mambo wanayoyaona kama viongozi, wakianza kufirikia kuwa wanafanyiwa fitina na kuwaeleza wachezaji kuwa wanaonewa, watakuwa wameingia kwenye mtego wa Etoile na watashindwa kufanya vizuri.

Hata wakiingia uwanjani jumamosi wakiona kama mwamuzi hayuko upande wao, wacheze soka la kuwatoa wapinzani kwenye eneo lao, wasiwape upenyo mapema wa kuingia kwenye eneo la hatari, kwasababu wakifanya hivyo wachezaji wa Etoile wanaweza kujiangusha na kupewa penalti au faulo za mapema.

Ikitokea hivyo maana yake Yanga watakuwa na uwezekano wa kufungwa mapema na kuondoka mchezoni.


MPENJA BLOG inawatakiwa kila la kheri Yanga!



Maoni: 0712461976

0 comments:

 
https://www.sexmutant.com/ https://www.sexindrag.com/ porn movies sex videos hd porno video