Thursday, April 30, 2015

Maguri (kushoto) akiwa na Awadhi Juma

MSHAMBULIAJI mwenye nguvu na kasi wa Simba, Elius Maguri amesema kamwe hawezi kukataa tamaa kutokana na kitendo cha kocha mkuu wa klabu hiyo, Mserbia Goran Kopunovic kumuweka benchi watoto wa mjini wanaita 'kochoma mahindi' katika mechi za ligi kuu Tanzania bara zinazoendelea kurindima wat

Simba imebakiza mechi mbili tu za ligi kuu dhidi ya Azam fc jumapili hii na JKT Ruvu mei 9 mwaka huu na sahizi ipo nafasi ya tatu ikijikusanyia pointi 41 baada ya kucheza mechi 24, pointi nne nyuma ya Azam fc waliocheza mechi 23.

Hata hivyo Maguri aliyekuwa kipenzi cha kocha aliyeondoka Simba, Patrick Ackson Phiri ameiambia MPENJA BLOG kuwa hana uhakika wa kucheza mechi hizo na yeye mwenyewe amekiri kutozifikiria

“Kwenye mpira wa miguu kuna wakati unapata nafasi na wakati mwingine hupati, kila mwalimu ana falsafa yake, lakini mimi siwezi kukata tamaa, napambana, nafanya mazoezi kwa bidii”. Amesema Maguri na kuongeza: “Kama Mungu atajaalia tukawa pamoja msimu ujao, watu watarajie mambo mazuri. Hutajawi kukaa na mwalimu Kopunovic (Goran) kuzungumza kuhusu suala langu, lakini ni mwalimu mzuri, anajua kufundisha, mhamasishaji, pamoja na kufundisha timu vizuri, kikubwa kwake anajua namna ya kuhamasisha”.

Mshambuliaji huyo wa zamani wa Tanzania Prisons na Ruvu Shooting aliyesajiliwa na Simba majira ya kiangazi mwaka jana amesema kwasababu mechi zimebaki mbili hataki kuzungumzia kwanini hatumiki, lakini msimu mpya utakapoanza itabidi ajue mstakabali wa kupata nafasi ya kucheza.


“Najisikia vibaya sana tunapopoteza mechi halafu mimi nataka nicheze kuisaidia timu yangu, inauma sana ukizingatia nilisajiliwa ili niisaidie timu yangu, lakini wanaingia wachezaji 11 na wengine wanabaki wa akiba, mwalimu yeye ndiye anaona nani acheze na nani abaki”.

Maguri mpaka sasa ameifungia Simba magoli matatu (3) msimu huu.

0 comments:

 
https://www.sexmutant.com/ https://www.sexindrag.com/ porn movies sex videos hd porno video