Wednesday, April 29, 2015

MSHAMBULIAJI wa Yanga, Daniel ‘Danny’ Davis Mrwanda amefichua siri kwamba yeye si mchezaji wa Yanga tu bali ni shabiki wa timu hiyo toka enzi za utoto wake.
Mrwanda amefanya mahojiano maalumu na mtandao huu baada ya kutwaa ubingwa wa ligi kuu kwa mara ya kwanza tangu aanze kucheza soka nchini.
Mshambuliaji huyo wa zamani wa Simba, Polisi Morogoro amesema msimu wa 2009/2010 ambao Simba walichukua ubingwa bila kufungwa mechi yoyote chini ya Patrick Phiri alitoa mchango mkubwa, lakini dakika za mwisho akaondoka kwenda Vietnam kucheza soka la kulipwa hivyo hakuvaa medali siku Simba wanakabidhiwa ubingwa.
Mwishoni wa juma lilipopita Yanga walitazwa mabingwa rasmi baada ya kuifunga Polisi Moro magoli 4-1 na kufikisha pointi 55 amabazo haziwezi kufikiwa na timu yoyote na wana mechi mbili mkononi dhidi ya Azam na Ndanda fc.

MAHOJIANO YA MTANDAO HUU NA DANNY MRWANDA

Swali: Umesikiaje kuwa sehemu ya mafanikio ya kutwaa ubingwa ndani ya klabu ya Yanga?


Mrwanda: Hakuna kitu kizuri kama kuona kitu ulichokuwa unakitumikia kwa muda mrefu halafu kimefanikiwa, timu ya Yanga imetwaa ubingwa, hii ni timu yangu, nimefurahi sana. Ni vigumu kujua nini mtu anawaza moyoni mwake, lakini inafikia wakati inabidi uzungumze hisia za moyoni mwako, mimi naipenda Yanga siku zote.
Swali: Ulianza kuipenda Yanga ukiwa na umri gani?

Mrwanda: Katika maisha kuna vitu vinakuja bila kupanga, siwezi kusema nilianza kuipenda Yanga nikiwa na umri gani, lakini naipenda sana Yanga.

Swali: kitu gani kikubwa kilikufanya uipende Yanga na si timu nyingine?


Mrwanda: Unajua si kitu nadharia, sisi tunakua katika familia ambazo tayari kuna watu waliokutangulia, utakuta kuna wazazi au mtu yeyote wa ‘kitaa’ anaizungumzia timu fulani na wewe mwenyewe unajikuta umeingia moja kwa moja kwenye mfumo ule ule.

Swali: Mshambuliaji gani wa siku za nyuma aliyewahi kuichezea Yanga na ukamkubali?


Mrwanda: Nilikuwa namkubali sana ‘Braza’ Lunyamila (Edibily), alikuwa ananifurahisa sana, nilikuwa namfuatilia sana, ni mtu aliyenivutia sana.

Swali:Kuna maneno ya mtaani kwamba mchezaji huyu ni mpenzi wa timu fulani na anacheza chini ya kiwango anapokutana na timu anayoipenda, wewe una mtazamo gani juu ya hilo?

Mrwanda: Mimi siwezi kumpinga mtu yoyote kuhusu hilo, ndio maana nimewashukuru mashabiki, sio wote wanaofanya hivyo, wengi walikuwa hawaamini kama mimi nipo pale kwa ajili ya kuitumikia timu moja kwa moja, ukweli ni kwamba huu ni mpira, kuna wakati unashuka na kupanda, ni mambo ya kimpira, unaona hata wachezaji wa ulaya kuna wakati wanapitia mazingira magumu, lakini haimaanishi labda mtu haipendi timu fulani

Swali: Ni mara yako ya ngapi kuvaa medali ya VPL hapa nchini?


Mrwanda: Itakuwa mara ya kwanza yangu japo katika timu nilizopitia nilishawahi kusaidia timu ikapata ubingwa lakini dakika za mwisho nikaondoka, mfano nilipokuwa Simba msimu wa 2009/2010 tukiwa na kocha Patrick Phiri, tulichukua ubingwa bila kufungwa, lakini nikaondoka mwishoni mwa msimu nikaenda Vietnam.

Swali: Ushindi huu unaupeleka kwa nani?



Mrwanda:  Naupelekea kwa familia yangu, kwanza kwa mwanangu mdogo wa kike, ni jambo zuri, ni mwaka ambao amezaliwa na tukio kubwa limetokea, ingawa niliwahi kuvaa medali nchi nyingine nilizowahi kucheza, hapa nyumbani ndio mara yangu ya kwanza, najisikia furaha sana.

0 comments:

 
https://www.sexmutant.com/ https://www.sexindrag.com/ porn movies sex videos hd porno video