Thursday, February 19, 2015

DSC_0302BAADA ya michezo minne ugenini kikosi cha Mbeya City Fc kinarejea kwenye uwanja wa Sokoine jijini Mbeya  jumapili hii kuivaa Yanga ya Dar  es Salaam katika mfululizo wa  kindumbwendumbwe cha ligi kuu ya soka Tanzania Bara  huu ukiwa ni mchezo wa ‘kiporo’ baada ya kuahirishwa awali kufuatia uwepo wa michuano ya kombe la Mapinduzi.
Akizungumza kuelekea mchezo huu Kocha wa City Juma Mwambusi amesema kuwa anafahamu uzito  wa mechi hiyo hasa ukizingatia matokeo yaliyokuwepo msimu uliopita baina ya timu hizo hivyo kwa namna yoyote mchezo utakuwa mgumu kwa kuwa City itacheza ikiwa na shauku ya kulipa kisasi cha kupoteza mchezo wa mzunguko wa pili msimu uliopita.
“Huu utakuwa ni moja ya michezo migumu tutaingia uwanjani tukiwa na kumbukumbu ya kupoteza mchezo wetu  wa pili dhidi yao msimu uliopita, tulianza ligi vibaya  msimu huu  hasa katika michezo saba ya mwanzo, mara hii tuko vizuri  ndiyo maana tuliweza kuifunga Simba nyumbani,najua utakuwa mchezo mgumu lakini matokeo ndiyo kitu pekee tunachokihitaji hivi sasa” alisema
Akiendelea zaidi Mwambusi alisema kuwa City imekuwa nje ya jiji la Mbeya  takribani wiki nne ikicheza michezo ya ligi na kufanikiwa kushinda mmoja, ikitoka sare miwili na kupoteza mmoja jambo ambalo limewafanya wachezaji kuwa na ari kubwa ya kutafuta matokeo kwenye mchezo wa jumapili.
DSC_0192Katika hatua nyingine nahodha Hassani Mwasapili amesema  nyota wote ndani ya kikosi wako vizuri na wana ari kubwa kuelekea mchezo wa jumapili wanachosubiri ni muda kufika ili kuidabisha  Yanga
“Wachezaji wote wako vizuri kila mmoja ana ari kubwa, tunataka kushinda mchezo huu ili kuwahakikishia mashabiki wetu kuwa hatukubahatisha kuifunga Simba  kwenye uwanja wa Taifa” alisema Mwasapili.

0 comments:

 
https://www.sexmutant.com/ https://www.sexindrag.com/ porn movies sex videos hd porno video