Thursday, February 19, 2015

 Yanga na Simba ndio timu zinazobeba  taswira ya soka la Tanzania

 Na Oswald Ngonyani


KATIKA vitu ambavyo nchi ya Tanzania imebarikiwa ni pamoja na kuwa na idadi kubwa ya wapenda michezo hususan mchezo wa soka.


Lakini pamoja na kuwa na idadi kubwa ya wanazi na mashabiki wa mchezo huo kwa bahati mbaya sana watanzania walio wengi wanaonekana kuihususudu zaidi soka ya nje kuliko soka yetu watanzania.


Pengine kunaweza kukawa na sababu lukuki za watanzania wengi kuwa na utamaduni huu lakini miongoni mwa sababu ambazo zipo wazi zaidi ni Ubora wa Ligi za wenzetu, Ligi ambazo kwazo zipo imara kutoka ngazi ya Uongozi wa juu mpaka kwa Uongozi wa timu husika.


Mbali na suala la uongozi, pia uwezo wa hali ya juu unaooneshwa na wachezaji na vilabu husika ni sababu nyingineyo ambayo kwa kiasi kikubwa imewafanya wadau na wanazi wengi wa soka la bongo kuwa wafuasi wakubwa wa soka ya Ulaya, soka ambayo kila leo inazidi kujiongezea idadi ya mashabiki.


Wakati fulani nilikuwa ninawaza kuhusu hawa wachezaji tulio nao sasa, Je ni kweli kabisa uwezo wao ni wa chini sana hata washindwe kuleta ubora katika ligi zetu mbalimbali hasa Ligi Kuu ya Vodacom?


Je ni kweli Viongozi tulio nao ndiyo haswa sababu ya soka letu watanzania kuzidi kurudi nyuma badala ya kusonga mbele kama ilivyo kwa wenzetu kule Ulaya na kwingineko?


Je, Uongozi wetu wenye dhamana ya mpira wa miguu nchini (TFF) ni kweli ndiyo chanzo cha madudu haya yanayoonekana kutokea kila leo katika soka la bongo?

 


Azam fc inaaminika kuwa klabu yenye mtazamo mpya katika sola la Tanzania


Pengine kila mwanafamilia ya mchezo wa soka atakuwa na jawabu lake kuhusu maswali haya niliyouliza.  Mimi naweza nikasema mfumo mbovu wa kiutendaji ndani ya Ligi ndiyo sababu ya madudu haya yanayojitokeza kila leo, lakini mwingine anaweza akasema mambo mengine ambayo pia yanaweza yakawa sababu ya soka letu kuzidi kuwa na uswahili mwingi.


Kwa siku za karibuni Ligi yetu imeonekana kuboreshwa sana na wadhamini wake, na wengi walidhani kuwa baada ya maboresho hayo pengine ustahimilivu na ubora wa Ligi yetu vingezidi kujipambanua lakini kwa bahati mbaya ni kama tunazidi kudorora.


Kasi ya wachezaji wetu kwenda kufanya majaribio (trials) ughaibuni wala haipo tena. Wanandinga wetu wameonekana kutokuwa na mipango thabiti kuhusu kutafuta maslahi yao hata nje ya mipaka.


Wapo wapo tu, wala hawaeleweki. Leo hii ukiwauliza wachezaji wengi wa soka la bongo kuhusu malengo yao kwa siku za baadaye kuhusu Uanasoka wao, wengi watakujibu majibu ambayo yanawiana.


Kucheza Simba, Yanga au Azam ndizo ndoto za wachezaji wetu hawa, na wale ambao tayari wapo katika vikosi hivi vya timu kubwa na zinazolipa vizuri, wamekwishabweteka na wala hawaiwazii kesho yao kunako mustakabali wa kutengeneza pesa kupitia vipaji vyao.

SHANGILIA5

Mbeya City fc ni timu yenye mtazamo wa kisasa ingawa bado ni changa

Wakati mwingine sioni sababu sana ya kuwashangaa mashabiki wa mchezo wa kandanda hapa nchini kuamua kujikita zaidi katika soka la Ughaibuni, pengine wamekwishaona kariba ya wachezaji wetu wengi, wachezaji ambao soka yao ni ile ile, wala haileti hamasa kuitazama.


Wachezaji wetu wanacheza mchezo unaofanana karibu kila kitu. Katika michezo kumi ambayo utafuatilia kwa umakini hutaweza kugundua vipaji vya ziada walivyonavyo wachezaji wetu hawa.


Mtibwa Sugar ni moja ya timu zilizokaa muda mrefu katika ligi ya Tanzania bara

Asilimia kubwa ya wachezaji tulio nao wanacheza mpira wa “Mam’bomba” yaani aina ya mpira wa kubutua butua, mpira ambao hata mtu asiyekuwa na’idea’ ya mchezo wa soka anaweza akafanya hivyo. 

Yaani kuucheza mpira katika minajili ya ‘bora liende’.


Ni jambo linalotia hasira sana lakini hakuna namna nyingine kwani haya yote yanayotokea katika soka la sasa yapo kwa sababu ya vile mfumo wetu ulivyo.

Wachezaji wetu hawajipi nafasi ya kuwafuatilia wachezaji wenzao wanaocheza soka la kulipwa kule Ulaya.


Wachezaji ambao wanaupa heshima kubwa mpira, hii ni kutokana na ukweli kuwa kupitia soka wanaweza kuyaendesha maisha yao tena kwa mafanikio makubwa.


Wanafanya vema pale wanapopata nafasi ya kusajiliwa timu fulani lakini pia pale wanapopata nafasi dimbani. Si watu wa kubweteka kama ilivyo kwa wachezaji wetu.


Ndio maana wachezaji kama Cristiano Ronaldo na Lionel Messi siku zote wanaonekana kuwa bora na hata kuukwaa uchezaji bora wa dunia mara kwa mara hii inatokana na heshima wanayoitoa katika mchezo huu.


Hawana dharau, wala hawawezi kubweteka kwa sababu ya mafanikio waliyo nayo sasa.Wanaendelea kujibidiisha tena na tena kwa lengo la kukidhi haja ya uhitaji kwa mashabiki wao kitu ambacho wachezaji wa Kitanzania wamekishindwa.


Soka la bongo michosho mitupu. Soka la bongo linakinaisha na kwa kiasi kikubwa linakera tena linakera sana. Viongozi wanaongoza soka pasipo kufuata misingi stahiki ya kiuongozi.


Wachezaji nao hali kadhalika, wala hawaoneshi kuiheshimu kazi yao hiyo. Wapo wapo tu wala hawana tofauti na watu wengine.Viongozi wa timu nao wana hulka zilezile, hulka za kutojitambua za kuongoza timu katika minajili ya bora liende.

Kwa staili hii ni lazima tutapunguza mashabiki na hata kuwapa mwanya wakuwa wafuasi wakubwa wa soka ya nje, vinginevyo ni lazima Viongozi husika wafanye kazi ya ziada ili kuifanya Ligi yetu kuwa bora zaidi, lakini pia wachezaji wetu wanatakiwa kuwatendea haki mashabiki wao tofauti na ilivyo sasa.


MIMI YANGU MACHO

(0767 57 32 87)


0 comments:

 
https://www.sexmutant.com/ https://www.sexindrag.com/ porn movies sex videos hd porno video