Wednesday, February 18, 2015


Paris Saint-Germain striker Zlatan Ibrahimovic believes his side have a 'good chance' of going through
Mshambulizi wa Paris Saint-Germain, Zlatan Ibrahimovic anaamini wataitupa nje Chelsea

MSHAMBULIAJI wa Paris Saint-Germain, Zlatan Ibrahimovic anaamini timu yake ina nafasi nzuri zaidi ya kutinga robo fainali ya ligi ya mabingwa barani Ulaya.
Wapinzai wao Chelsea walipata faida ya goli la ugenini katika sare ya 1-1 jana usiku uwanja wa Parc des Princes, shukuruni kwa bao la Branislav Ivanovic, lakini Ibrahimovic anajiamini kuwa kikosi chake kitapata matokeo mazuri Stamford Bridge.
Akizungumzia sare ya jana dhidi ya vinara wa EPL, Chelesea, Ibrahimovic amesema: "Tuko katika nafasi nzuri ya kusonga mbele. Mchezo bado uko wazi".
Chelsea manager Jose Mourinho shakes hands with Ibrahimovic after the final whistle 
Kocha wa Chelsea, Jose Mourinho akisalimiana na Ibrahimovic baada ya kipyenga cha mwisho 

"Tulionesha kuwa tunaweza kutengeneza nafasi nyingi. Sio kazi rahisi ligi ya mabingwa. Wana wachezaji wakubwa. Huu ndio mpira. Tunahitaji kuomba bahati. Ngoja tusubiri kuona kocha atataka tuchezaje mechi ya marudiano". Amesema Ibrahimovic.

0 comments:

 
https://www.sexmutant.com/ https://www.sexindrag.com/ porn movies sex videos hd porno video