Thursday, February 19, 2015

MABINGWA watetezi wa ligi kuu soka Tanzania bara, Azam fc wamelazimisha suluhu (0-0) ugenini dhidi ya wenyeji Ruvu Shootings katika mechi ya ligi kuu soka Tanzania bara iliyomalizika jioni hii uwanja wa Mabatini, Mlandizi, Pwani.

Kwa dakika zote 90’ timu zote zilicheza soka la uangalifu na kuzuia mianya ya kufungwa goli.

Ruvu Shootings walikuwa makini zaidi katika mechi ya leo kuhakikisha hawagawi pointi tatu kama walivyofanya msimu uliopita walipofungwa 3-0 na Azam fc katika uwanja wao.

Awali walitamba kuwazuia Azam fc kupata pointi tatu kwa kuwafunga na katika mechi leo, lakini wamefanikiwa kufanya kupata pointi moja.

Dakika za lala salama timu zote zilitengeneza mipango ya kufunga magoli, lakini makipa wa timu zote walisimama imara.

Dakika ya 80’ ya mchezo, John Bocco aliachia shuti kali, lakini mlinda mlango wa Shootings, Rashid Abdallah alipangua na mabeki wakaondosha mpira eneo lao la hatari.

Dakika ya 82’ Michael Aidan almanusura awafungie Shootings kwa mpira wa adhabu, lakini shuti lake likaokolewa na kipa Aishi Manula na kuwa kona ambayo haikuzaa matunda.

Mpaka dakika 90’ zinamalizika, Ruvu Shootings 0 Azam fc 0.

Azam walifanikiwa kupiga mashuti 7 yaliyolenga lango dhidi ya 6 ya Ruvu Shootings .

Pia Azam walimilika mpira kwa asilimia 52 kwa 48 za Ruvu Shootings.

Kwa matokeo hayo, Azam FC wamefikisha pointi 26 kileleni wakisubiri matokeo ya Mbeya ambapo Yanga wanaongoza mabao 2-0 mpaka sasa.

Azam fc wamebaki na magoli yao 22 ya kufunga na 12 ya kufungwa, hivyo wastani wa mabao ya kufunga na kufungwa ni 10.

Ruvu Shootings wao wamefikisha pointi 20  na kupanda mpaka nafasi ya 5 kutoka ya 9.


Nafasi ya nne inaendelea kushikiliwa na Simba wenye pointi 21.

0 comments:

 
https://www.sexmutant.com/ https://www.sexindrag.com/ porn movies sex videos hd porno video