Onyo kali: Rais UEFA, Michel Platini ametoa tamko lake juu ya maisha ya soka la kimataifa ya Franck Ribery
RAIS wa UEFA, Michel Platini ametishia kumfungia mechi tatu Franck Ribery kama atakataa kujiunga na timu ya taifa ya Ufaransa-licha ya ukweli kwamba mshambuliaji huyo wa Bayern Munich amestaafu soka la kimataifa.
Ribery aliyekosa fainali za kombe la dunia mwaka 2014 kutokana na majeruhi, alitangaza kustaafu soka la kimataifa mwezi wa nane mwaka huu.
Hata hivyo Platini anadai maamuzi ya Ribery kustaafu soka la kimataifa yako mikononi mwa kocha wa Ufaransa Didier Deschamps kwani ndiye mwenye maamuzi ya mwisho kuchagua kikosi.

Hapa ndio nyumbani: Ribery anataka kuelekeza nguvu zote katika klabu yake ya Bayern Munich inayoshiriki ligi kuu nchini Ujerumani maarufu kama Bundesliga

Mkwara mzito: Platini ameweka wazi kuwa hatima ya soka la kimataifa kwa Ribery liko mikononi mwa kocha wa Ufaransa Didier Deschamps
0 comments:
Post a Comment