Monday, August 18, 2014

Ibrahim Mwaipopo 

Na Baraka Mpenja, Dar es salaam

NDANDA FC ya mkoani Mtwara imegoma kujiamini kufanya maajabu katika michuano ya ligi kuu soka Tanzania bara msimu ujao mithiri ya Mbeya City fc, lakini itajitahidi kadiri iwezavyo kuleta ushindani.

Kocha msaidizi wa klabu hiyo, Ngawina Ngawina amesema kuwa kwasasa wanaendelea na mazoezi ambapo wachezaji wanaonekana kuimarika siku hadi siku, ingawa ni mapema kutabiri kuwa watafanya makubwa katika msimu wao wa kwanza wa ligi kuu kwasababu mpira ni mchezo unaohitaji maandalizi zaidi.

Ngawina alisema mpira wa miguu ni mchezo wa hadharani na timu yenye maandalizi mazuri na mipango thabiti inapata matokeo mazuri, hivyo kwa kutambua hilo wanaendelea kwa umakini na programu ya mazoezi, wakianzia mazoezi magumu na sasa wanaendelea na mambo ya kimbinu na kiufundi.

Ndanda fc inayoungwa na mashabiki wengi wa mkoani Mtwara imesajili wachezaji wapya na Ngawina amethibitisha kuwanasa wanandinga wawili wenye uzoefu.

“Mambo yanakwenda vizuri. Tumekamilisha usajili na tumeongeza wachezaji wawili wenye uzoefu, Thomas Morris na Ibrahim Mwaipopo”. Alisema Ngawina.


“Tumekamilisha hatua ya kwanza ya usajili na kama tutaona kuna mapungufu tutaongeza wachezaji wengine wakati wa dirisha dogo”

“Mwaipopo ni mchezaji ambaye hakutumika sana na klabu ya Azam fc msimu uliopita kutokana na mipango ya mwalimu, lakini bado ni mchezaji mzuri anayeweza kuisaidia timu yetu.”

‘Morris tumekuwa naye katika mazoezi, msimu uliopita alicheza Kenya na sasa amerudi nyumbani, uzoefu wake utatusaidia sana.”

“Ndanda fc tunasema tutajitahidi kwa kadiri tuwezavyo kuhakikisha tunafanya vizuri ligi kuu. Jumatano tutacheza mechi ya kirafiki dhidi ya Mtibwa Sugar katika uwanja wa Bandari, hivyo itakuwa nafasi nzuri ya kukipima kikosi chetu.’

Ndanda fc ni miongoni mwa timu tatu zilizopamba ligi kuu msimu ujao, nyingine ni Polisi Morogoro na Stand United ya Shinyanga.


Timu zilizoshuka daraja msimu uliopita ni Rhino Rangers ya Tabora, JKT Oljoro ya Arusha na Ashanti United ya Ilala, jijini Dar es salaam.

0 comments:

 
https://www.sexmutant.com/ https://www.sexindrag.com/ porn movies sex videos hd porno video