Saturday, August 16, 2014

Afisa habari na Mawasiliano wa Shirikisho la soka Tanzania, Boniface Wambura Mgoyo

Na Baraka Mpenja, Dar es salaam


Imechapishwa Agosti 16, 2014, saa 1:00 mchana

KLABU za Ligi Kuu ya Vodacom (VPL) na Ligi Daraja la Kwanza (FDL) zimeendelea kukumbushwa kuwasilisha orodha ya watendaji wa mabenchi yao ya ufundi yakiongozwa na Kocha Mkuu katika Ofisi za Shirikisho la soka Tanzania, TFF.

 Afisa habari na mawasiliano wa TFF, Boniface Wambura Mgoyo alisema ni wajibu wa klabu kuhakikisha zinatekeleza maagizo hayo kwani ni matakwa ya Kanuni za VPL na zile za FDL.

“CV ni sehemu ya kanuni za ligi. Kabla ya ligi kuanza tunahitaji kuona vyeti vya makocha wataoongoza timu za ligi kuu na daraja la kwanza.” Alisema Wambura.

“Timu kama haina kocha anayekidhi kanuni, itakaa bila kocha kwenye benchi lake la ufundi kwa mechi nne.”

Hata hivyo, Wambura alikiri kuwa zoezi hilo halijakamilika kutokana na kubadilisha mfumo wa uwasilishaji ambapo sasa klabu zinatuma orodha ya watendaji wake wa benchi la kwa njia ya kompyuta.

“Tumebadili mfumo wa uwasilishaji ambapo sasa wanatumia kompyuta zao. Kwasasa hatuwezi kujua ni kwa kiasi gani kumekuwa na mwitikio, lakini wameendelea kututumia na kama kuna matatizo tunawasiliana nao”.


Wambura alitoa wito kwa klabu za ligi kuu na ligi daraja la kwanza kuendelea kutekeleza agizo hilo la kikanuni kabla ya kuanza kwa msimu mpya wa ligi.

0 comments:

 
https://www.sexmutant.com/ https://www.sexindrag.com/ porn movies sex videos hd porno video