Saturday, August 16, 2014

Katibu mkuu wa Shirikisho la soka Tanzania, Selestine Mwesigwa

Na Baraka Mpenja, Dar es salaam

Imechapishwa Agosti 16, 2014, saa 6:56 mchana

ZIARA ya Magwiji wa Real Madrid nchini Tanzania inayotarajia kuanza Agosti 22 mwaka huu imezidi kuvuta hisia za mashabiki wa kabumbu ndani na nje ya nchi.

Magwiji hao watakaoongozwa na wanasoka waliowahi kutamba katika ulimwengu wa soka kwenye michuano ya La Liga, UEFA na kombe la dunia wakiwa na Real Madrid pamoja na kombe la dunia wakiwa na nchi zao watacheza mechi ya kirafiki Agosti 23 mwaka huu uwanja wa Taifa jijini Dar es salaam dhidi ya kikosi maalumu cha ‘Tanzania All Stars’.

Miongoni mwa wachezaji wanaotarajiwa kuwepo ni mwanasoka bora wa dunia wa zamani, Mfaransa Zinedine Zidane, Fabio Cannavaro, Luis Madeila Figo na Ronaldo De Lima.

Kuelekea katika ziara hiyo ya kihistoria, Shirikisho la soka Tanzania, TFF, limefurahishwa kuingia katika historia ya klabu kubwa duniani ya Real Madrid ambao kwasasa ndio mabingwa wa ligi ya mabingwa barani Ulaya.

Katibu Mkuu wa TFF, Selestine Mwesigwa alisema hii ni nafasi muhimu katika maendeleo ya soka la Tanzania na kama fursa hii itatumika vizuri basi italeta matunda mazuri.

“TFF tunaingia katika historia ya Real Madrid. Nafasi hii ni muhimu katika kuwahamasisha vijana wetu kuwa kumbe mpira unaweza kuendelea hata baada ya kustaafu”. Alisema Mwesigwa.

“Kuna masuala tutajifunza hususani kwa wachezaji wetu wanaostaafu mpira. Kustaafu soka si sababu ya kuacha moja kwa moja kujihusisha na maendeleo ya michezo na kujihusisha na shughuli nyingine za kijamii.”

“Utalii na uchumi wa nchi hii pia utakuwa na kitu cha kufaidika katika ziara hii’.

“Wito wangu kwa klabu kongwe za Simba na Yanga ni kutumia nafasi hii kama chachu ya kuwakumbuka wachezaji wao wa zamani."

0 comments:

 
https://www.sexmutant.com/ https://www.sexindrag.com/ porn movies sex videos hd porno video