Wednesday, August 20, 2014

Na Baraka Mpenja

AZAM FC wanashuka dimbani leo kukabiliana na El Merreikh ya Sudan katika mchezo wa robo fainali ya klabu bingwa Afrika mashariki na kati, Kombe la Kagame inayondelea mjini Kigali Rwanda.

Mechi hiyo kali na ya kukata na shoka itaanza mapema saa 9:00 alasiri.

Taarifa kutoka Kigali zinaeleza kuwa mechi hiyo imevuta hisia za mashabiki wengi wa soka kutokana na ubora na viwango vya timu hizo katika mashindano hayo.

Timu zote mbili zinapewa nafasi ya kutwaa ubingwa, hivyo mchezo wa leo kuonekana kama fainali iliyokuja mapema.

Meneje wa Azam fc, Jemedari Said amesema wachezaji wote wameamka salama na wana morali kubwa ya kufanya vizuri ikizingatiwa walitembelewa na Naibu Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo, Juma Suleiman Nkamia na kumuahidi kupigana kufa na kupona.

Jemedari alisema wachezaji wote wapo salama na hakuna majeruhi yeyote,nah ii ni nafasi nzuri kwao kocha mkuu, Mcameroon, Joseph Marius Omog  kuamua nani aanze.

“Kila kitu kipo sawasawa na katika mazoezi ya mwisho jana wachezaji wote walifanya walikuwepo,” alisema Jemedari. “Kwetu ni kama fainali iliyotujia mapema kwasababu ya namna El Merreikh wanavyocheza kiufundi na kimbinu.”

“Unapozungumzia El Merreikh, unazungumzia moja kati ya timu nane bora barani Afrika na wamekuwa wakicheza mara kwa mara hatua ya makundu ya ligi ya mabingwa, kwahiyo unapoitaja timu hiyo unataja timu kubwa.”

Mechi nyingine ya Robo fainali itawakutanisha KCC ya Uganda  dhidi ya Altabara ya kusini.

Polisi ya Rwanda ilifanikiwa kufuzu hatua ya nusu fainali jana baada ya kuifunga kwa penalti 9-8 Atletico ya Burundi.

Hii ilitokana na timu hizo kumaliza dakika 90 kwa suluhu pacha ya bila kufungana. Hivyo Polisi na APR watakutana nusu fainali.


Nao maafande wa APR waliwatoa Rayon Sport kwa penalti 4-3 baada ya dakika 90 kumalizika kwa sare ya 2-2.

0 comments:

 
https://www.sexmutant.com/ https://www.sexindrag.com/ porn movies sex videos hd porno video