Tuesday, August 5, 2014

 Na Baraka Mpenja, Dar es salaam

Imechapishwa Agosti 5, 2014, saa 5:00 asubuhi

BARAZA la vyama vya mpira wa miguu Afrika Mashariki na kati, CECAFA limeiengua rasmi klabu Yanga kushiri kombe la Kagame 2014 na nafasi yake imechukuliwa na mabingwa wa ligi kuu soka Tanzania bara, Azam fc.

Tangu awali, CECAFA walitoa taarifa kuwa Azam watapewa nafasi ya upendeleo katika michuano hiyo inayoanza kushika kasi Agosti 8 mwaka huu, mjini Kigali nchini Rwanda, lakini mpaka jana wana Lambalamba walikuwa hawana taarifa rasmi.

Yanga sc ndio walitakiwa kushiriki michuano hiyo, lakini waliamua kupeleka kikosi B ambapo CECAFA ilikikataa na kuitaka timu hiyo ya makutano ya Twiga na Jangwani, Kariokoo jijini Dar es salaam ipeleke kikosi cha kwanza pamoja na kocha mkuu, Mbrazil Marcio Maximo.

Mpaka jana usiku, Yanga walikuwa hawajathibitisha kukubaliana na agizo hilo la CECAFA na taarifa zilizoripotiwa na mtandao huu usiku wa jana ni kwamba Yanga wamegoma kubadili kikosi chao, hivyo hawatashiriki.

Baada ya Yanga kushindwa kutii Agizo la CECAFA, viongozi wa baraza hilo wakatuma taarifa TFF wakiagiza timu nyingine iliyo tayari ipeleke  kikosi na ndipo Azam waliosemwa tangu mwanzo kuwa watashiriki kupata nafasi hiyo.


Azam wamekubali kwenda kushiriki kwasababu walihitaji nafasi hiyo na watatuma kikosi kilichotwaa ubingwa msimu uliopita cha wachezaji 20 pamoja na wachezaji wote wapya iliyowasajili.

Kikosi kilichotumwa Kigali na Azam FC ni: Makipa Mwadini Ally, Aishi Manula.

Mabeki: Shomary Kapombe, Gadiel Michael, Waziri Salum, Abdalallah Kheri, Aggrey Morris, David Mwantika na Said Mourad.

Viungo: Mudathir Yahya, Kipre Balou, Salumu Abubakar, Himid Mao, Khamis Mcha ‘Vialli’, Farid Musaa na Joseph Peterson.

Washumbuliaji: Didier Kavumbagu, Kipre Tchetche,  Leonel Saint-Preux na John Bocco.

Washambuliaji wawili, Ismail Diara kutoka Mali na Gaudens Mwaikimba wameachwa katika kikosi hicho.

Benchi la Ufundi litaongozwa na kocha mkuu Mcameroon, Joseph Marius Omog, kocha msaidizi Kalimangonga Ongala, kocha wa makipa Idd Abubakar na meneje, Jemadari Said.


Azam fc wanaingia kundi A na kuungana na Wenyeji, Rayon Sport, Coffee kutoka Ethiopia, Atlabara ya Sudan kusini na KMKM ya Zanzibar.

0 comments:

 
https://www.sexmutant.com/ https://www.sexindrag.com/ porn movies sex videos hd porno video