Tuesday, July 8, 2014

Oliver Bierhoff, wa pili kutoka kushoto,  aliifungia bao la kwanza timu yake katika fainali za Euro za mwaka 1996 kati ya Ujerumani na Jamhuri ya Czech, moja ya kombe la karibu la kimataifa ambalo Ujerumani wameshinda.
Oliver Bierhoff anajua jinsi ya kushinda kombe. Mshambuliaji huyo wa zamani wa AC Milan mwenye miaka 46 aliifungia goli la ushindi Ujerumani katika fainali za Euro za mwaka 1996 kwenye mchezo wa fainali dhidi ya Czech Republic ndani ya uwanja wa Wembley.

Bierhoff, meneja mkuu wa timu ya taifa ya Ujerumani, ametumia muda wake kuongea kwa njia ya simu na mtandao wa ESPN FC akizungumzia mchezo wa nusu fainali wa usiku dhidi ya wenyeji Brazil, hususani akizungumzia nafasi ya Ujerumani na jinsi watakavyotumia teknolojia kuwafunga wapinzani wao.

Raphael Honigstein: Mr. Bierhoff, vipi morali ya kambi kuelekea mchezo wa nusu fainali dhidi ya Brazil Brazil?

Oliver Bierhoff: Timu iko imara, timu iko tayari. Nimekuwepo kwenye mashindano mengi, kama mchezaji na meneja mkuu, lakini sijawahi kuona timu ambayo inashangilia kidogo baada ya kushinda robo fainali. Kwa asilimia kubwa wana malengo, hawataki safari kufika mwisho. Nadhani safari ya Rio (kwa ajili ya mchezo wa Ufaransa) pia ilisaidia kwasababu nilimpa kila mchezaji majukumu kuwa tunatakiwa kufika fainali Maracana. Utulivu umekuwa mkubwa, lakini kuna hali ya ugumu wa mchezo kidogo.

RH: Hakuna anayetaka kucheza mechi ya mshindi wa tatu. Je, kombe la dunia mwaka huu litapimwa kama mafanikio ya Ujerumani hata kama hawatafika fainali?

OB: Kwangu mimi , ndiyo. Tunataka kushinda kombe kwa gharama yoyote. Lakini kitu chochote kinaweza kutokea katika mchezo wa nusu fainali au fainali. Unaweza kuwa katika kiwango chako kikubwa na bado ukapoteza. Au unaweza kushinda kwa bahati. Tofauti ya timu hizi mbili ni ndogo. Yote kwa yote, ninachoweza kusema wachezaji kwa kweli wanahitaji kushinda kombe.

RH: Unautazamaje mchezo dhidi ya Brazil?

OB: Watakuwa wapinzani wagumu, hata kama hawana Neymar na Thiago Silva. Watacheza pamoja kama timu. Wataalam wetu wameitazama Brazil kwa miaka minne. Tuna data kutoka kwenye michezo yao bila Silva na Neymar. Tumewaonesha vijana wetu namna ya kuwashinda Brazil.

Tumefanya maarifa na kuweka takwimu hizi katika simu. Data zinapatikana kirahisi na wanajua ni mchezaji gani atakuwa mshambuliaji badala ya Neymar, kwa mfano tunaweza kuwaambia mabeki juu ya wachezaji wawili au watatu wanaoweza kumbadili. Hii imetusaidia sana.
 RH: Unaweza kutupa mfano mwingine jinsi ambavyo wachambuzi wa mpira wanatumiwa na timu ya Ujerumani nchini Brazil?
OB: Tuligundua kuwa wachezaji wanapenda kuwasiliana kwa vifaa vyao vya kiteknolojia. Kwahiyo kwa msaada wa wataalam wetu wa teknolojia, tulikuja na mfumo ambao unatusaidia kutupa vipande vya video za uchambuzi kwa mchezaji mmoja mmoja au makundi ya wachezaji kutoka timu mbalimbali. Kila mchezaji anapata mifano mingi ya jinsi alivyocheza vabaya na vizuri baada ya mechi. Wanaweza kutazama kwa muda wao na kuangalia takwimu za viwango vyao. Hii imetusaidia sana kuliko kuonesha mkanda wa video wa dakika 90. Wachezaji wanafurahia hali hii na wanatoa mrejesho mzuri.Pia tuna takwimu mbalimbali za wapinzani wetu. Jérôme Boateng aliombwa kumtazama Cristiano Ronaldo jinsi anavyotembea akiwa katika eneo la boksi, huo ni mfano mwingine. Na kabla ya mchezo dhidi ya Ufaransa, tuliwaona Ufaransa wakiwa watulivu eneo la kiungo, lakini maeneo ya pembeni yalikuwa na udhaifu kwasababu mabeki wao wa pembeni walikuwa hawapandi vizuri. Kwahiyo tulitumia nafasi hizo.

RH: Je,  mnajiamini tangu muwafunge Ufaransa?, ukitazama matokeo ya 2-1 dhidi ya Algeria pia yaliibua wasiwasi mkubwa.


OB: Wasiwasi huu ulizushwa nje ya kambi, lakini ndani ya kambi hakuna tatizo. Moja ya kazi yangu ni kuwapa moyo wachezaji. Huwezi kuruhusu hisia za hofu zikaja karibu yako, hususani kutoka nje ya timu. Baada ya ushindi wa mabao 4-0 dhidi ya Ureno katika mchezo wa ufunguzi. Nilitoa ruhusa ya kupiga simu kwa yeyote anayetaka kujadili kwa namba gani tunaweza kushinda kombe la dunia. Siku kadhaa baadaye, baada ya sare ya 2-2 na Ghana, kila mtu alikuwa na wasiwasi. Maneno haya yalikuwa na athari na yalitufanya tubadilike kila mchezo. Huwezi kujitenga kutokana na haya. Tumeweza kufanya vizuri, kwa mtazamo wangu. Na wakati mwingine, nimekuwa nikiwaambia wachezaji: Huu ni mchezo—huu ni mchezo.

0 comments:

 
https://www.sexmutant.com/ https://www.sexindrag.com/ porn movies sex videos hd porno video