
Imechapishwa Julai 4, 2014, saa 3:47 asubuhi
KOCHA wa Colombia, Jose Pekerman
anatarajia kuwaona Brazil wakiwa katika kiwango chao bora kuelekea katika mchezo wa robo fainali ya kombe la
dunia utakaopigwa kuanzia majira ya saa 5 usiku wa leo.
The Selecao wamekuwa wakikosolewa na
vyombo vya habari vya nchini mwao kwa kiwango chao `mbofu mbofu` katika
mashindano ya mwaka huu, hususani baada ya kupata ushindi wa kubahatisha wa
mikwaju ya penati dhidi ya Chile hatua ya 16.
Pekerman hatarajia kuwaona wenyeji
wakiwa na presha baada ya mchezo wa Fortaleza
dhidi ya Chile.
“Kufuzu nusu fainali ni matarajio
makubwa na kila timu itacheza kwa kiwango chake cha juu ili kupata nafasi hiyo”.
“Kwa timu zote mbili tunaweza kuona
wachezaji wakubwa, na wachezaji wakubwa wanapokuwepo timu zote, mechi inakuwa
na mvuto mkubwa”.
Inajadiliwa nchini Brazil kuwa
matumaini makubwa ya wenyeji kufuzu, yanaweza kuwapa nafasi Colombia kufuzu pia,
japokuwa Pekerman hawezi kuyaamini maneno hayo.
“Timu yetu mara zote inaangalia mbele,”
alieleza. “Kwa Colombia, kila mechi ni changamoto mpya. Kwahiyo hatuwezi
kutazama nyuma kwa kile tulichofanya. Jambo la msingi ni kutojihisi kama tuna
nafasi. Tutauchukuliwa mchezo huu kama tulivyocheza mechi za nyuma”.

0 comments:
Post a Comment