
Diego Simeone anaweza kuondoka Atletico Madrid majira ya kiangazi mwaka huu, huku akiwavutia watu wengi.
Imechapishwa Julai 4, 2014, saa 3:13 asubuhi
DIEGO Simeone ndiye kocha aliye kwenye moto kwasasa na anaongoza kupigiwa upatu wa kutwaa kazi ya ukocha mkuu wa timu ya taifa ya Hispania kama Vicente del Bosque anaachia au kama kocha wa Argentina, Alejandro Sabella atashindwa katika mechi ya robo fainali ya kombe la dunia dhidi ya Ubelgiji.
Simeone mwenye miaka 44 ameingia katika orodha ya makocha wanaosakwa sana baada ya kuonesha kiwango cha juu akiwa na Atletico Madrid ambapo alitwaa ubingwa wa La Liga na alifika fainali ya UEFA.
Muargentina huyo anaweza kwenda kuiongoza nchi yake, lakini taarifa kutoka vyanzo vya karibu na Simeone vinasema kuwa ana matarajio makubwa ya kuiongoza Hispania.

Simeone anaweza kumfundisha Messi na Argentina wakati huu hatima ya baadaye ya Alejandro Sabella ikiwa mashakani.

Kocha mpya? Hispania wameanza mipango ya kutafuta mrithi wa Vicente Del Bosque.
Maamuzi ya hatima ya Del Bosque yameshafikiwa na kuteuliwa kwa Simeone kutamfanya kuwa kocha wa kwanza wa kigeni kuifundisha Hispania kwa zaidi ya nusu karne.

0 comments:
Post a Comment