
Imechapishwa Julai 12, 2014, saa 6:46 mchana
WAKATI umewadia. Mara nyingi kumekuwepo na mjadala wa nani mkali kati ya Diego Maradona na Lionel Messi. Wengi wanasema Messi hajashinda kombe la dunia, lakini jumapili ya kesho nahodha huyo wa Argentina anaweza kumaliza kila kitu.
Nyota huyo mwenye miaka 27 itasimama kwa dakika 90 tu zitakazoweza kumfanya kuwa mchezaji mkubwa zaidi duniania ambaye ameweka kila aina ya rekodi, makombe, magoli na vinginevyo.

Mfungaji huyo wa muda wote wa Barcelona akiwa na mabao 354, Messi ameshinda makombe 21 akiwa na wakatalunya, ni mchezaji pekee katika historia kutwaa tuzo ya mwanasoka bora wa dunia (Ballons d`Or) mara nne mfululizo na pia aliongeza medali ya dhahabu ya Olympic na kombe la dunia la vijana chini ya miaka 20 akiwa na jezi za taifa lake. Kuna kitu kimoja tu kinakosekana.

Mfungaji huyo wa muda wote wa Barcelona akiwa na mabao 354, Messi ameshinda makombe 21 akiwa na wakatalunya, ni mchezaji pekee katika historia kutwaa tuzo ya mwanasoka bora wa dunia (Ballons d`Or) mara nne mfululizo na pia aliongeza medali ya dhahabu ya Olympic na kombe la dunia la vijana chini ya miaka 20 akiwa na jezi za taifa lake. Kuna kitu kimoja tu kinakosekana.
Kama alama ya taifa, Maradano aliiongoza Argentina mwaka 1986, naye Messi anacheza fainali yake ya kwanza ya kombe la dunia dhidi ya Ujerumani.
Bado watu wanabishana kuwalinganisha wakali hao kwa kuangalia utaifa wao, staili moja ya uchezaji na magoli mengi waliyofunga, lakini kiukweli, Messi amepata mafanikio makubwa zaidi ya kocha huyo wa zamani wa Argentina kwa ngazi ya klabu hasa unapoangalia magoli na makombe.
0 comments:
Post a Comment