Saturday, June 28, 2014



Afisa habari wa Yanga sc, Baraka Kizuguto (kushoto) akiwa na Coutinho (kulia) baada ya kuwasili  nchini  jana akitokea kwao nchini Brazil

Na Baraka Mpenja, Dar es salaam

0712461976

Imechapishwa Juni 28, 2014, saa 4:00 asubuhi

YANGA SC imemsajili kiungo mshambuliaji kutoka nchini Brazil, Andrey Marcel Ferreira Coutinho.

Mchezaji huyo aliwasili jana mchana jijini Dar es salaam akitokea kwao nchini Brazil tayari kwa kuanza kazi ya kuitumikia Yanga katika msimu wa 2014/2014 wa ligi kuu soka Tanzania bara.

Coutinho aliwaeleza waandishi wa habari kuwa anajisikia furaha kuwa Tanzania, nchi ambayo watu wake wanapenda mpira.

Mchezaji huyo haijui Tanzania, lakini ameifahamu kutokana na bosi wake Marcio Maximo ambaye amechangia kwa asilimia zote kumleta nchini.

Bila shaka wakati wanaongea na Maximo juu ya kuja kufanya kazi Tanzania, Coutinho alihoji mambo mengi na mazingira ya Tanzania na kupewa majibu na Maximo ambaye unaweza kusema ni mwenyeji wake.

Maximo anafahamu utamaduni wa mashabiki wa Tanzania na alimweleza ukweli kiungo huyo na yeye kuiamini Tanzania mpaka kusema anafurahia kufanya kazi kwenye ardhi ya nchi hii ya Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete.

Brazil kuna wachezaji wengi na vipaji vingi vya soka. Hii ni nchi inayosemekana kunukia mpira kila kona.

Tunaona wabrazil wengi wanafanya makubwa katika soka la sasa duniani, lakini miaka ya nyuma walitokea wachezaji wakali pia.
Unamkumbuka Pele? Huko mbali, miaka ya karibuni tu, akina Ronaldo, Ronaldinho, Ricardo Kaka`, Robinho, na sasa Neymar wametikisa soka la dunia.

Hawa ni mfano tu, ukiamua kuwataja wachezaji wa Brazil waliofanya kazi nzuri utaandika kwa muda mrefu na huwezi kumaliza,  lakini ninachojaribu kusema ni kwamba, Brazil ni nchi yenye vipaji vingi vya soka.

Kwa wale waliobahatika kufika Brazil, wanajua wazi kuhusu hilo. Ukipita mitaa mingi ya nchi hii, lazima uwakute vijana wanacheza soka.

Katika maelezo ya Coutinho alisema amewahi kucheza barani Asia na alipata uzoefu mzuri, hivyo anaamini chini ya makocha aliowazoea ataisaidia Yanga.

Kucheza Asia sio jambo jepesi, huko pia kuna mpira na watu wana mipango mizuri.
 http://ilkhabergazetesi.tv/wordpress/wp-content/uploads/2013/06/10_numara_brezilyada_bulundu_h2705.jpg
Anaujua Mpira?: Coutinho anaanza mazoezi jumatatu chini ya kocha Marcio Maximo.
Watu wengi wanabeza suala la Yanga kumsajili Coutinho. Maneno ya kejeli yanasikika hasa kutoka upande wa pili. Utasikia Coutinho sio mchezaji, muuza `madafu` tu huko Brazil.

Wengine wanahoji, angekuwa mchezaji mzuri si angecheza huko huko Brazil?, kwanini aje Yanga, tena Tanzania huku ambako mpira tunautafuta kwa `tochi`.

Kuna kitu kimoja lazima tukumbushane, katika maisha ya mwanadamu, kuna matabaki makubwa matatu.

Kuna tabaka la juu, la kati na la chini, yawezekana likawepo la chini kabisa.

Ukiingia kiuchumi, tabaka la juu unazungumzia watu wenye mkwanja mrefu, tabaka la chini ni wale wanaofuatia, la chini ni wale wenzangu na mimi, la chini kabisa, huko kuna balaa.

Hata katika mpira, kuna matabaka ya wachezaji, wapo wa kiwango cha juu, hapa unataja akina Lionel Messi, Cristiano Ronaldo, Luis Suarez, Wayne Rooney, Andrea Pirlo, Karim Benzema na wengi wengi ambao siwezi kuwataja.

Pia kuna tabaka la kati, hapa ndio kuna wachezaji wengi, barani Ulaya, Amerika kusini, Amerika kaskazini, Asia na kwingineko.

Kuna tabaka la chini. Hapa kuna wachezaji wengi pia kutoka mabara yote.

Lipo tabaka la chini kabisa, huku sasa kuna wachezaji wengi wanaosaka nafasi za kusogea mbele. Yawezekana katika viwango vya dunia, Watanzania tukawa kwenye tabaka hili.

Lakini kuna tofauti kati ya mchezaji wa tabaka la chini wa Brazil na wa Tanzania. Tofauti hii inaweza kutokana na kiwango cha taifa katika viwango vya FIFA.

Mchezaji wa mtaani nchini Brazil, Hispania, Ujerumani anaweza kuwa na kiwango cha juu zaidi ya Mrisho Ngassa, John Bocco, Ramadhan Singano, hawa ni mfano tu, sina nia mbaya.

Sisemi Coutinho anaweza kuwa mkali zaidi ya wachezaji wote wa Tanzania eti tu kwasababu anatoka Brazil, lakini najaribu kueleza kuwa dharau kabla ya kumuona mtu akicheza sio jambo la busara.

Yawezekana yakawa ni maneno ya watani wa jadi kwasababu yamezoeleka, lakini dhana ya kumdharau mchezaji kabla ya kumuona lazima izungumzwe.

Binafsi sijawahi kumfuatilia mchezaji huyu kwa undani, ingawa nina habari zake kidogo. Lakini hainipi sababu ya kusema atawafaa Yanga au hapana.

Kinachotakiwa ni kusubiri kumuona anafanya mazoezi chini ya Maximo, na uwezo wake utaonekana hadharani.

Mpira wa miguu ni mchezo wa hadharani, kama Coutinho ni mkali, wote tutamuona kuanzia jumatatu.

Lakini tahadhari lazima iwepo, kumuona kwenye mazoezi kwa siku mbili tatu sio sababu ya kusema hafai au anafaa. Mpira una mambo mengi, leo hii anaweza kuchemsha, lakini kesho akafanya vizuri.

Suala la kumpa muda ni muhimu. Lazima aangaliwe zaidi. Siamini kama Maximo kambeba bila kumjua. Yeye ni kocha na kufundisha mpira ni kazi yake, hawezi kuleta mtu atakayemharibia kazi.

Coutinho kwa bahati nzuri amegundua kuwa atakabiliana na changamoto zikiwemo za kimazingira. Lakini Maximo lazima amemwambia tabia ya mashabiki wa Kibongo.

Unaweza kufanya kazi nzuri, lakini ukaharibu kwenye mechi ya watani wa jadi, ukaambulia kusasambuliwa na kutukanwa.
 
Big Bosi! Marcio Maximo (kushoto) akizungumza na waandishi wa habari jana jijini Dar es salaam

Sio wakati muafaka wa kumuita Coutinho muuza `madafu` Brazil, lazima aheshimike na tusubiri kuona vitu vyake.

Hawezi kuwa kama Oscar, Neymar, Willian, Fred. Nilisema kuna matabaka katika maisha ya soka. Hata kama ni wa kiwango cha chini, lazima ukumbuke wewe uko tabaka gani.

Unajua Yanga kwanini haiwezi kumsajili Neymar au Oscar? Kwasababu ipo tabaka la chini kulinganisha na Barcelona na Chelsea.

Mbuzi hula kutokana na urefu wa kamba yake, Yanga wanamuweza Coutinho, waacha wamtumie. Wenyewe wakiona anafaa wataendelea naye, wakiona `Galasa` watatangaza kumuacha. Mpira sio vita.

Cha msingi tusubiri kuona Coutinho ana nini, baada ya hapo tutapata cha kuandika na kuzungumza.

Sina maslahi na Yanga wala Coutinho, nina maslahi na soka la Tanzania. Sipendi kuzungumza kitu ambacho sijakiona. Huwezi kutabiri mchezaji Fulani muuza `madafu` au mkali wakati kichwani mwako huna hata kumbukumbu ya kumuona akicheza.

“Coutinho welcome in Tanzania” ukutane na mashabiki wa Kibongo ulioambiwa wanapenda mpira. Kweli wanapenda, lakini suala la uvumilivu kidogo limewapiga chenga ya mwili.

0 comments:

 
https://www.sexmutant.com/ https://www.sexindrag.com/ porn movies sex videos hd porno video