Saturday, May 24, 2014



 http://2.bp.blogspot.com/-9oG8isschLg/UDh2SMShyGI/AAAAAAAAEKU/No4A0rwDX6g/s400/OMEGA+SEME.jpg
Na Baraka Mpenja, Dar es salaam

Imechapishwa Mei 24, 2014, saa 11: 56 jioni

KIUNGO wa Dar Young Africans,  Omega Seme, amesema kwasasa hana muda wa kupoteza zaidi ya kufanya mazoezi makali ya kujiweka fiti tayari kwa kuitumikia klabu yake msimu mpya wa ligi kuu soka Tanzania bara unaotarajia kuanza kutimua vumbi mwezi Agosti mwaka huu.
Akizungumza na MPENJA BLOG jioni hii, Omega aliyekuwa anacheza kwa mkopo Tanzania Prisons msimu uliopita  amesema kuwa anafahamu Yanga kuna viungo bora, lakini imani yake ni kupata namba ya kudumu kutokana na maandalizi anayoyafanya kwa sasa.
“Kupata namba inategemea na mwalimu. Yeye ndiye anajua. Cha msingi ni kujiweka fiti, mwalimu akiona ninafaa basi atanipa namba”. Alisema Omega.
Omega aliongeza kuwa uwepo wa Hassan Dilunga na Haruna Niyonzima katika nafasi ya kiungo ni changamoto kubwa kwake, lakini hana wasiwasi kwasababu anajiona mwenye uwezo mkubwa wa kupambana nao.
Kiungo huyo aliwaondoa hofu mashabiki wa Yanga juu ya kurejea kwake na kuwataka kuwa na subira ili kumuona akiwa katika kiwango cha hali ya juu.
Kurejeshwa kwa Omega kwa asilimia kubwa kumetokana na kuondoka kwa kiungo mahiri wa Yanga sc, Frank Domayo aliyejiunga na mabingwa watetezi wa ligi kuu soka Tanzania bara, Azam fc.
Akizungumzia kuongezeka kwa vijana katika timu za ligi kuu, Omega alisema ni jambo jema na anaomba timu zizidi kuwaamini makinda kwasababu wana uwezo wa hali ya juu.
“Vijana wapewe nafasi kwasababu wanaweza kuzisaidia timu zetu na timu ya Taifa”. Alisema Omega.
Kuhusu Taifa stars, Omega alikiri kutamani kuichezea kwasababu timu hiyo  kwasasa ni nzuri na ina wachezaji wazuri.
“Stars inacheza vizuri. Nikipata nafasi nitafurahi kuitumikia nchi yangu”.

0 comments:

 
https://www.sexmutant.com/ https://www.sexindrag.com/ porn movies sex videos hd porno video