Saturday, May 24, 2014



 bukos (2)
Na Baraka Mpenja, Dar es salaam

Imechapishwa Mei 24, 2014, saa 4: 24 asubuhi

TIMU ya taifa ya vijana wenye umri chini ya miaka 20 ya Tanzania (Ngorongoro Heroes) inatarajia kushuka dimbani leo jijini Kaduna katikati ya Nigeria katika mchezo wa marudiano dhidi ya timu ya taifa ya Nigeria (Flying Eagles). 
Ngorongoro wataingia uwanjani wakiwa na kumbukumbu ya kufungwa mabao 2-0 katika mechi ya kwanza iliyopigwa uwanja wa Taifa jijini Dar es salaam wiki mbili zilizopita. 
Kocha mkuu wa timu hiyo, John Simkoko anahitaji kuiongoza Ngorongoro kupata ushindi wa mabao 3-0  ili kusonga mbele, au mabao 2-0 ili vijana wajaribu bahati yao kwenye mikwaju ya penati. 
Kocha Simkoko alikaririwa akiwa jijini Dar es salaam akisema bado kikosi chake kina matumaini ya kufanya vizuri licha ya kimahesabu kuonekana ni ngumu kwa Ngorongoro kufuzu hatua inayofauta. 
Nigeria walionesha kiwango kikubwa katika mchezo wa kwanza na walitawala maeneo yote. Walioneokana kujiamini, kumiliki mpira na kucheza kama wapo uwanja wa nyumbani.
Waliwazidi Ngongoro uzoefu na walitumia vyema makosa ya vijana wa Tanzania.
Nigeria ni moja ya nchi zinazotisha kwa soka la vijana barani Afrika, lakini kwenye mpira wa miguu lolote linaweza kutokea.
Cha msingi vijana wa Ngorongoro wasikate tamaa mapema na kuona mambo hayawezekani. Wacheze kwa nguvu na kuamini kuwa wanaweza kufunga mabao 3-0.
Mechi ya ugenini itakuwa na presha kwa timu ya Tanzania, lakini Simkoko ni mwalimu mzoefu na anaweza kuwatuliza vijana wake.
Mwamuzi Alhadi Allaou Mahamat wa Tchad ndiye atakayechezesha mechi hiyo. Atasaidiwa na Issa Yaya, Alfred Madjihoudel na Idriss Biani wote kutoka Tchad. Kamishna ni Aboubakar Alim Konate wa Cameroon.
Kila la kheri Ngorongoro Hereos katika mchezo wenu wa leo.

0 comments:

 
https://www.sexmutant.com/ https://www.sexindrag.com/ porn movies sex videos hd porno video