Saturday, May 24, 2014



 http://1.bp.blogspot.com/-eS4uaRKjA4Y/UjWrRwt7Y3I/AAAAAAAAwC4/jFrQDx9PAbE/s640/1.jpg
Na Baraka Mpenja, Dar es salaam

Imechapishwa Mei 24, 2014, saa 11:00 asubuhi

WASHAMBULIAJI  wa kimataifa wa Tanzania, Mbwana Ally Samata na Thomas Emmanuel Ulimwengu kesho jumapili wanatarajia kuiongoza TP Mazembe katika mchezo wa hatua ya makundi ya ligi ya mabingwa barani Afrika dhidi ya wapinzani wao wakubwa, AS Vita mjini Lubumbashi.

Timu hizi hasimu zitakutana katika mchezo wa kesho zikiwa na kumbukumbu ya kusababisha maafa ya vifo vya watu zaidi ya 15 katika mchezo wao wa ligi kuu ya DR Congo wiki za karibuni.

Tukio hilo baya lilitokea mjini Kinshasa baada ya mashabiki wa AS Vita kutoridhishwa na kipigo cha bao 1-0 kutoka kwa wapinzania wao TP Mazembe.

Mchezo wa kesho umevuta hisia za mashabiki wengi wa soka, kwani timu hizi zinapokutana, upinzani unakuwabmkubwa mno nje ya uwanja na ndani ya uwanja.

TP Mazembe wataingia katika mchezo wa kesho wakiwa na kumbukumbu mbaya ya kupigwa bao 1-0 kwenye mchezo wao wa kwanza  wa kundi A na  Al Hilal ya Sudan mnao mei 17 mwaka huu.
 http://1.bp.blogspot.com/-eK5M-2ZU2Ww/Up3ImvQEYaI/AAAAAAAACSM/sgwkzPGbY40/s640/Samata-Bwana.jpg
Mei 18 mwaka huu, AS Vita walitumia vyema uwanja wao wa nyumbani baada ya kuilaza Zamalek ya Misri mabao 2-1, hivyo wataingia katika mchezo huo wa kundi A wakiwa na morali kubwa ya kusaka ushindi wa pili.

Mechi nyingine ya kesho jumapili itakuwa ya Kundi B kati ya wenyeji  ES Setif ya Algeria dhidi ya SC Sfaxine ya Tunia.

Mei 18 mwaka huu SC Sfaxine waliifumua Al Ahly Benghazi ya Libya mabao 3-1, wakati mei 17, 2014, ES Setif waliifunga mabao 2-1 Esperance ya Tunisia. 
Mbali na mechi hizo za kesho, leo hii mitanange mingine inaendelea ambapo kundi A, wenyeji Zamalek watawakaribisha Al Hilal kutoka nchini Sudan.

Huu utakuwa mchezo muhimu kwa Mafarao waliopoteza mechi iliyopita. Al Hilal wao watakuwa wanahitaji ushindi wa pili katika michuano hiyo.

Mechi ya kundi B leo hii,  wenyeji Al Ahly Benghazi ya Libya waliopoteza mechi ya kwanza kwa mabao 3-1 watakabiliana na  miamba ya soka la Tunisia, Esperance ambao nao mechi ya kwanza walilala kwa mabao 2-1.

0 comments:

 
https://www.sexmutant.com/ https://www.sexindrag.com/ porn movies sex videos hd porno video