Friday, May 23, 2014



http://www.tplboard.co.tz/assets/uploads/files/273f8-63.jpg
Na Baraka Mpenja, Dar es salaam

Imechapishwa Mei 23, 2014, saa 10:36 jioni

BAADA ya kunusurika kushuka daraja msimu uliopita, maafande wa Mgambo JKT kutoka jijini Tanga wanatarajia kuanza kambi yao juni 9 mwaka huu tayari kwa maandalizi ya msimu mpya wa ligi kuu soka Tanzania bara.
Kocha msaidizi wa klabu hiyo, Moka Shaban Dihimba amezungumza na MPENJA BLOG na kueleza kuwa malengo ya kuingia kambini mapema ni kukwepa majanga ya msimu uliopita ambapo waliponea chupuchupu kurudi ligi daraja la kwanza.
“Tutabaki na wachezaji wote. Hatuachi mtu, lakini tunatarajia kuongeza nguvu hususani safu ya ushambuliaji”. Alibainisha  Moka.
“Timu ilivyosajiliwa mara ya kwanza sisi hatukuwepo. Tulipoingia makocha wapya tulijitahidi kuhakikisha timu haishuki daraja, lakini kuna nafasi tumeona tunahitaji kurekebisha ili tusifanye vibaya kama ilivyotokea msimu uliopita”.
Moka aliongeza kuwa wakirudi kambini mwezi ujao, wataalika wachezaji kutoka sehemu mbalimbali ili kuwafanyia majaribio kama baadhi ya timu zifanyavyo.
Aidha, alisisitiza kuwa msimu ujao wanahitaji kuonesha makali kama Mbeya City fc kwasababu mechi za mwishoni mwa msimu walivuna pointi nyingi na ilidhihirisha kuwa mambo yanawezekana.
‘Katika majaribio ya wachezaji tutazingatia umri. Hatutahaingaika na wachezaji waliotoswa na timu nyingine.”
“Ukichukua vijana wadogo unaweza kukaa nao misimu miwili mpaka mitatu. Ukichukua wakongwe unaweza kukaa nao msimu mmoja na wakachoka”. Alisema Moka.

0 comments:

 
https://www.sexmutant.com/ https://www.sexindrag.com/ porn movies sex videos hd porno video