Wednesday, May 28, 2014



 IMG_9208
 Na Baraka Mpenja, Dar es salaam

Imechapishwa Mei 28, 2014, saa 8:55

MAAFANDE wa Polisi kutoka visiwani Zanzibar jana wameondolewa katika michuano mipya Ya CECAFA Nile Basin Cup baada ya kufungwa mabao 3-0 dhidi ya Victoria Universty ya Uganda .
Huo ulikuwa mchezo wa tatu kwa Polisi kupoteza na wemeondolewa kwa kufungwa mabao 9 katika mechi tatu bila kufunga hata goli moja.
Walipoteza michezo miwili  iliyopita kwa kufungwa idadi ya mabao kama ya jana dhidi ya Malakia FC na Al Merreikh.
Katika mchezo mwinge hapo jana, Malakia walifungwa mabao 4-2 dhidi ya wenyeji Al Merreikh.
 DSCF5413
Michuano hiyo inatarajia kuendelea leo jioni na usiku ambapo majira ya saa 11:30 jioni kwa saa za Afrika mashariki, wawakilishi wa Tanzania bara, Mbeya City fc watakuwa wanaisaka nafasi ya kucheza robo fainali ya michuano hiyo kwa kukabiliana na Etincelles mjini Khartoum.
Mbeya City walioanza michuano hiyo kwa kuibuka na ushindi wa mabao 3-2 dhidi ya Academie ya Burundi na mechi ya pili kufungwa mabao 2-1 na AFC Leopard, wanahitaji ushindi kwa namna yoyote ile ili kufuzu hatua ya robo fainali.
Baadaye usiku majira ya 2:00 usiku, AFC Leopard watakabiliana na ACademie Tchite.
Mjini Sandi, wenye Al –Shandi watakuwa kibaruani dhidi ya Defence ya Ethiopia.

0 comments:

 
https://www.sexmutant.com/ https://www.sexindrag.com/ porn movies sex videos hd porno video