Friday, May 30, 2014



Na Baraka Mbolembole

Imechapishwa Mei 30, 2014, saa 12:45 asubuhi

Neno ' Kujiuzulu' lina maana mbili. Ni kuacha, au kuachia, kazi, haki, madai, au mali. Ni kuacha kufanya jambo, kuachia au kuachana na kusalimu amri, kukata tamaa; kusema kuwa mtu hatibiki au tatizo Fulani linakushinda kutatua. Ni kutoa kwa...., au kumuachia mwingine mwenye uwezo au mamlaka, hasa kwa kudaiwa au kulazimishwa. Kujiuzulu, ni kusalimu amri ya adui ya kujitolea. Maelezo haya ndiyo maana ya kwanza ya neon Kujiuzulu.
Maana ya pili, Ni kuwa tayari kukubali na kustahimili; kukubali kuwa jambo Fulani ni lazima liwe, halizuiliki. Ni kukubali kuwa umeshindwa au utashindwa, na kuwa tayari kustahimili matokeo ya kushindwa. Kujiuzulu, ni kukubali kusalimu amri ya adui au mpinzani wako na kuwa tayari kustahimili matokeo yake. Ni kukubali kutekwa, na kuwa tayari kustahimili matokeo ya kuwa mateka. Kujiuzulu ni kukubali kushindw. Kujiuzulu ni kukubali kustahimili matokeo ya kukata tamaa na kushindwa jambo!.
Wakati anachuku fomu kasha kurudisha, Michael Wambura alikuwa mwanachama halali wa klabu ya Simba SC. Kama sivyo hakupaswa kupewa fomu za kugombea nafasi ya urais katika uchaguzi mkuu wa klabu hiyo unaotaraji kufanyika, juni 29. Wambura anafahamu kuwa wanachama wa Simba wanataka mabadiliko, wanahitaji mapinduzi ya kweli, na mapinduzi hayo yatawezeka na kama wanachama wenyewe wa klabu watasimama kwa umoja katika kuhitaji mabadiliko hayo. Kama mtu atatumia silaha ambayo haitoi nafasi ya kurudisha nyuma maendeleo anaweza kuibomoa ' ngome ' ya wapinga mapinduzi.
Sababu zote zilizotolewa ambazo zimemfanya, Wambura ' kuchinjiwa bahari' na kamati ya uchaguzi ya klabu hiyo chini ya wakili, Damas Ndumbaro, zinaweza kuwa na mashiko ila haziwezi kuficha udhaifu mkubwa uliopo katika kamati mbalimbali zinazokuwa na dhamana ya kusimamia chaguzi mbalimbali katika taasisi za soka. Naamini, Wambura aliingia mwenyewe katika uchaguzi huku akifahamu vita iliyokuwa mbele yake ilikuwa ikionesha ushindi kwa wapinzani wake ambao wanashindwa kukubali ' msamaha aliouomba' kutokana na kitendo chake cha kuipeleka klabu hiyo mahakani, mwaka 2010.
Kuna baadhi ya kikundi cha wanachama wa klabu hiyo kinaamini kuwa ndiyo wenye nguvu na mamlaka na wajuzi wa mambo, lakini sivyo, atawashinda tu siku moja kwa kuwa yupo mbele yao. Hata kama Wambura anachukiwa, lakini itabidi wakubali ukweli kwamba ' Wambura ana thamani ya uongozi', ni mtu makini, hodari na watu wanampenda. Ukitazama safu ya wagombea wa nafasi ya urais katika uchaguzi ujao wa klabu hiyo, Wambura ndiye mwenye uwezo. Amekata rufaa kupinga uamuzi huo wa kamati ya uchaguzi.
Simba haihitaji busara yake? Simba haihitaji juhudi yake ya kufanya kazi na uwezo wake wa kupata matokeo ?.Simba imekuwa ikiongozwa na ' wanakamati hodari' na si viongozi hodari. Simba imekamatwa na kikundi cha wafanyabiashara wabaya, na wenye nia ya kujikuza. Wakati, Jamal Malinzi alipoingia, TFF, rais huyo wa soka nchini alitangaza msamaha kwa wanasoka wote waliokuwa na adhabu za kawaida je, yeye hahusiki katika msahama huo?
Wambura inawezekana akawa mwanachama halali wa klabu, ama sivyo kama ilivyotangazwa na kamati ya uchaguzi, ila hawawezi kuficha udhaifu wao wa kushindwa kuthibitisha baadhi ya saini zilizopo katika nyaraka muhimu. Kama mtu anasema hajaweka saini, na ikaonekana saini yake. Hapo kuna tatizo na inawezekana kamati ya uchaguzi iliamua kukimbia na muda bila kufuatilia kwa umakini... Kamati hii ambayo inaongozwa na mwanasheria maarufu imekosa umakini, imeshindwa kujiamini, lakini mwisho wa siku imethibitika kuwa, Wambura ni mwanachama anayekubalika ndani ya klabu hivyo wanachama wengine wanaogombea uongozi wanatakiwa kupambana naye katika misingi ya demokrasia na sichuki binafsi.
Hawajiamini? Ndiyo, jibu lipo wazi tu, ila ukweli wanachama wa klabu wanahitaji kumuona katika orodha ya wagombea. Kujiuzulu, si muhimu ila kamati ya uchaguzi ya Simba inapaswa kusarenda kwakuwa imeshindwa kazi. Walimpaje fomu za kuwania nafasi muhimu kama si mwanachama?.Huyu mtu ana thamani ya uongozi, wanachama wa klabu ndiyo wenye kuamua kiongozi wamtakaye
0714 08 43 08

0 comments:

 
https://www.sexmutant.com/ https://www.sexindrag.com/ porn movies sex videos hd porno video