Friday, May 23, 2014



http://www.fullshangweblog.com/wp-content/uploads/2014/05/KIL-Henry_Josef_4253664a.jpg
Na Baraka Mpenja, Dar es salaam

Imechapishwa Mei 23, 2014, saa 10: 48 jioni.

KIUNGO mahiri aliyeichezea Simba sc msimu uliopita, Henry Joseph Shindika amesema bado hajazungumza na timu yoyote mpaka sasa kueleka msimu mpya wa ligi kuu soka Tanzania bara.
Joseph aliyemaliza mkataba na Simba mwishoni mwa msimu uliopita ameiambia MPENJA BLOG kuwa nia yake ni kuendelea kucheza ligi ya Tanzania msimu ujao, lakini hajui ataitumikia klabu gani.
“Kwasasa sijapata mchakato wowote, lakini kuna mambo nayaweka sawa, muda si mrefu nitawajulisha mashabiki wangu”. Alisema Joseph.
Kuhusu kucheza soka la kulipwa kwa mara nyingine, Joseph alisema bado hajapata timu yoyote, lakini kama itatokea nafasi ataondoka zake kusaka maisha mapya.
“Sijajua nitacheza wapi, mpira kazi yangu. Kokote kule nitaenda. Ikitokea nafasi nje nitaelekea huko”. Aliongeza Joseph.
Usajili wa majira ya kiangazi kueleka msimu wa 2014/2015 wa ligi kuu soka Tanzania bara unatarajia kufunguliwa rasmi juni 15 mwaka huu, lakini baadhi ya klabu kama Azam fc tayari zilishanasa majembe mapya.
Mabingwa hao wa ligi kuu soka Tanzania bara walishasajili wachezaji wawili kutoka Yanga, Frank Domayo `Chumvi` na Didier Kavumbagu.
Nao Yanga walishamuongezea mkataba beki wao kisiki, Mbuyu Twite aliyekuwepo katika rada za Azam fc.
Aidha, Joseph aliwatakia kila la heri Taifa stars kuelekea katika mchezo wa marudiano juni 1 mwaka huu mjini Harare dhidi ya wenyeji Zimbabwe.
“Kikubwa wachezaji wajitume tu. Wasijaribu kuwadharau Zimbabwe kwasababu lolote linaweza kutokea ugenini”. Alishauri Joseph.

0 comments:

 
https://www.sexmutant.com/ https://www.sexindrag.com/ porn movies sex videos hd porno video