Friday, May 23, 2014


http://2.bp.blogspot.com/-DMF8TI4QWgw/T9IdoAB1bDI/AAAAAAAAAD0/45_yRHt6oa4/s1600/Shadrack+Nsajigwa.JPG

Na Baraka Mpenja, Dar es salaam

Imechapishwa Mei 23, 2014 saa 11: 00 jioni

NAHODHA wa zamani wa klabu ya Yanga na timu ya taifa ya Tanzania, Taifa Stars, Shadrack John Nsajigwa Mwandemele amewataka wachezaji wa Taifa Stars kufuata maelekezo ya mwalimu wao na kuzingatia nidhamu ya mchezo katika mechi ya marudiano dhidi ya Zimbabwe, mjini Harare, juni 1 mwaka huu.
Taifa Stars iliyopata ushindi mwembamba wa bao 1-0 kwenye uwanja wa Taifa jijini Dar es salaam katika mechi ya kwanza kuwania kupangwa hatua ya makundi ya kusaka tiketi ya kucheza fainali za AFCON mwakani nchini Morocco, inahitaji sare ya aina yoyote ile au ushindi ili kusonga hatua inayofuata.
Mshindi wa jumla baina ya Taifa Stars na Zimbabwe atachuana na mshindi kati ya Msumbiji dhidi ya Sudan ya kusin, lakini mechi ya kwanza iliyopigwa mjini Maputo, Msumbiji walishinda kwa mabao 5-0, hivyo kuweka mguu nje-ndani.
Akizungumza na MPENJA BLOG, Nsajigwa alisema mechi za ugenini huwa ni ngumu kwasababu wenyeji  wanashambulia sana, hivyo ni jukumu la wachezaji wa Stars kujipanga na kuwa na nidhamu ya mchezo ili kupata matokeo mazuri.
“Kwasababu ni mechi ya ugenini, mwalimu aweke mkazo sana sehemu ya ulinzi. Lakini ushambuliaji pia ni muhimu kwasababu tunahitaji kushinda”. Alisema Nsajigwa.
“Mabeki wanaonekana kuzoeana kiasi, najua ni changamoto kwasababu mwalimu naye ni mgeni. Kila mchezaji awe na juhudi binafsi kwasababu mchezo utakuwa na presha kubwa”.
“Tuna goli moja, tunahitaji kulilinda. Nadhani wachezaji na mwalimu wao wanajua hilo”. Alisema Nsajigwa.
Beki huyo wa kulia wa zamani wa  Taifa stars aliyekuwa miongoni mwa walinzi waliokuwa wanaunda ngome bora ya Mbrazil Marcio Maximo na Jan Poulsen kwa nyakati tofauti aliongeza kuwa enzi zao walicheza kwa mafanikio sehemu ya ulinzi kwasababu walikaa kwa pamoja kwa muda mrefu.
“Kipindi chetu tulicheza  pamoja kwa muda mrefu. Tulizoeana sana na ndio maana tulikuwa hatufungwi. Pia tulikuwa na jitihada binafsi za kuisaidia timu”.
“Tulikuwa tunaelewana kwa kufuata mfumo wa mwalimu. Maximo alikuwa anatufundisha kulinda zaidi hasa mechi za ugenini.”
“ Stars ya sasa kuna mabadiliko ya mara kwa mara kwa wachezaji”. Alisema Nsajigwa.
Akizungumzia nafasi ya Stars kufuzu hatua ya makundi, Nsajigwa alisema bado safari ni ndefu na kama ikitokea tukafuzu basi itakuwa ni bahati.
Aidha, alisema ugeni wa mwalimu itaigharimu Stars kwa sasa, lakini ni muhimu kuanzia kwa kocha huyu ili timu iwe ya kudumu.
“Wachezaji wa timu ya taifa wanatakiwa kuondoka taratibu taratibu na sio kubadilishwa ghafla”.
‘Wawaache wazoeane. Wapewe muda. Wacheze mechi nyingi za kirafiki ili kuzoeana. Mara huyo kaingia mara katoka, hii haina tija kwa taifa”. Alifafanua Nsajigwa.

0 comments:

 
https://www.sexmutant.com/ https://www.sexindrag.com/ porn movies sex videos hd porno video