Friday, May 23, 2014



http://resources0.news.com.au/images/2013/08/02/1226690/420672-gi.jpg
NA DAVID NGALEMA

Imechapishwa Mei 23, 2014, saa 11:15 jioni

Siku chache zilizopita, Ryan Giggs alitangaza kustaafu soka. Atajiunga Luis Van Gaal kwenye benchi la ufundi la Man United kama kocha msaidizi.
Ni huzuni kubwa kutomuona tena dimbani akiwa na jezi yake namba 11, badala yake tutaendelea kumuona akiwa benchi na Luis Van Gaal . Sidhani kama ni sahihi kumpa mtu mwingine namba (11) ya Giggs aitumie , Sio kwa heshima tu, bali ni kwa mambo makubwa aliyoyafanya huyu jamaa akiwa Man United
Giggs ana historia ya kipekee katika ulimwengu wa soka, Ni mchezaji pekee aliyefunga goli kwenye kila msimu wa ligi kuu tangu aanze kucheza kwenye msimu wa 1990-91 mpaka 2013-14. Alifunga goli lake la kwanza kwenye Manchester Derby (nikimaanisha dhidi ya Man City), Manchester United ikishinda 1-0. Ikumbukwe kuwa alipitia Man City kabla ya kujiunga na Mashetani wekundu mwaka 1987.
Giggs ni mchezaji wa kwanza kushinda mfululizo tuzo ya Young player of the year mwaka 1992 na 1993, Wayne Rooney ni moja kati ya wachezaji waliowahi kushinda mara mbili mfululizo tuzo iyo.
Giggs katika historia yake aliweza kufunga magoli kadhaa ya kusisimua sana yakawa ni kati ya magoli bora ya msimu, lakini goli ambalo halitosahaulika milele ni lile alilowafunga Arsenal kwenye nusu fainali ya FA, akichukua mpira uliopotezwa na kiungo Patrick Viera kutoka katikati ya uwanja akipiga chenga kwa spidi na kwa kujiamini akikatiza katika ngome imara iliyoundwa na beki kama Tony Adams, Martin Keown na Lee Dixon na kuweka mpira nyavuni akimuacha David Seaman hana la kufanya langoni.
Akiwa Manchester United ameweza kushinda mataji makubwa mbalimbali kama UEFA champions league, EPL, FA. Msimu wake wa mwisho 2013-14 alikabidhiwa kuiongoza Man United katika mechi 4 zilizobakia baada kutimuliwa David Moyes. Kitendo cha Giggs kuaminika na kupewa nafasi hiyo, kinaonyesha yeye ni mtu wa aina gani. Ni ngumu kupata mtu kama Giggs tena kwenye ulimwengu wa soka.
Kuna tetesi kwamba kijana Adnan Januzaj anaweza kupewa jezi namba 11 ya gwiji Ryan Giggs. Sidhani kama huyo kinda anaweza kuvaa viatu vilivyoachwa na Giggs, Ni vikubwa mno. Januzaj anaweza kuwa ni mchezaji mzuri, lakini kila nikimuona uwanjani na namba 11, nitakua namkumbuka Ryan Giggs.
 Ningependa Januzaj asihusishwe na hii namba, inaweza kumuharibia mpira wake huyu bwana mdogo. Acha Januzaj awe Januzaj, aendelee kuvaa namba yake 44 au wampe namba nyingine lakini sio 11.
Ikiwa WestHam na Ac Milan waliweza kufuta jezi namba sita  kwa kuwaenzi Bobby Moore na Franco Baresi, Kwanini Man U wasifanye hivyo?
Hata Bongo, usitegemee kuona jezi namba 30 ikitumika tena Msimbazi, Hii ni kutokana maamuzi ya kuifuta ili kumuenzi marehemu Mafisango.
Mimi huwa namuita Sir Ryan Giggs, mwenye namba 11 mgongoni ya maajabu.
Imeandikwa na David Ngemela @muggypro. Mwanafuzi wa Chuo kikuu cha habari.

0 comments:

 
https://www.sexmutant.com/ https://www.sexindrag.com/ porn movies sex videos hd porno video