Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), Jamal Malinzi amewapongeza marais Davor Suker na Fouzi Lekjaa kwa kuchaguliwa tena hivi karibuni kuongoza mashirikisho ya mpira wa miguu katika nchi zao.
 Suker
 amechaguliwa tena kuwa Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu la Croatia 
(CFF) wakati Lekjaa amechaguliwa kuwa Rais wa Shirikisho la Mpira wa 
Miguu la Morocco (FRFM).
 Katika
 salamu zake za pongezi, Rais Malinzi amesema ushindi waliopata ni 
uthibitisho kuwa familia ya mpira wa miguu katika nchi zao ina imani 
kubwa kwao katika kuendeleza mchezo huo ndani na nje ya nchi hizo.
Rais
 Malinzi amesema Lekjaa na Suker wana uwezo wa kuendeleza kazi nzuri 
ambayo tayari imefanyika, lakini vilevile kuja na mawazo mapya ambayo 
yatakuwa changamoto kwa ustawi wa mchezo huo nchini Morocco na Croatia 
kwa ujumla.
BONIFACE WAMBURA
OFISA HABARI NA MAWASILIANO
SHIRIKISHO LA MPIRA WA MIGUU TANZANIA (TFF)

.jpg)



0 comments:
Post a Comment