Saturday, December 21, 2013

DSC_1384Na Baraka Mpenja wa Fullshangwe, Dar es salaam
Tel: 0712461976 au 0764302956
SHUGHULI pevu ya mechi ya `NANI MTANI JEMBE?` baina ya wekundu wa Msimbazi Simba, `Taifa Kubwa` dhidi ya watani wao wa jadi, Dar Young Africans, imemalizika jioni hii kwa Mnyama kuibuka na ushindi mnono wa mabao 3-1, kwenye uwanja wa Taifa, jijini Dar es salaam.
Simba waliocheza mpira safi na kuwazidi maarifa Yanga walioongozwa na nyota wao wote wameandika mabao yao kupitia kwa  kwa nyota wake Amis Tambwe aliyefunga mawili pamoja na kiungo Awadh Juma Issa.
Bao la wana Jangwani limefungwa na mshambuliaji wao Mpya Emmanuel Anord Okwi aliyeingia kuitumikia klabu hiyo kwa mara ya kwanza tanga asajili desemba 15 mwa huu akitokea klabu ya SC Villa ya Kampala Uganda.
Leo hii kiukweli, Yanga waliingia kwa kujiamini zaidi kutokana na kikosi chao kusheheni nyota wengi wakiwemo, Okwi, Kiiza, Ngassa, Didier Kavumbagu, Niyonzima na wengine wengi wenye majina.
Hata hivyo Yanga kama kawaida yao walicheza soka la kujiamini na kuonesha kuwa wanajua zaidi kupiga mpira wa burudani `Show Game`.
Simba wao waliingia kwa kazi moja ya kutafuta ushindi ikizingatiwa wamekuwa wakichukuliwa kirahisi na watani zao wa jadi kufuatia kuwa na mabadiliko mengi kikosini.
Simba walionakena kuwa dhaifu kwa maneno ya watu na nje ya uwanja, lakini wamecheza soka safi zaidi ya Yanga na kufanikiwa kuwafunga mabao hayo.
Juma Kaseja kaanza vibaya na  hii imeanza kuamsha maneno miongoni mwa mashabiki wa Yanga, lakini ni matokeo ya mpira, sema yamekuja wakati mbaya kwake.
Yawezekana baadhi ya mashabiki watawatupia lawama baadhi ya wachezaji, ila ni matokeo ya mpira na wamefanya makosa makubwa matatu na kufungwa.
Yanga kwa mara kadhaa walipata nafasi za kufunga, lakini kukosa umakini kumewagharimu.
Kwa upande wa  Ivo Philip Mapunda ameonekana kuimarika zaidi na kuwa bora kwa wakati wote.
Wakati watu wengi wakidai  Ivo kazeeka, leo hii imedhihirisha kuwa utu uzima dawa, kwani ameokoa michomo mingi zaidi kutoka kwa washambuliaji wa Yanga.
Amis Tambwe alisema lazima awafunge Yanga, hatimaye kwa mara ya kwanza  amefunga mabao mawili mawili muhimu katika ushindi mtamu kwa Mnyama.
Pia kocha mpya wa Simba SC, Mcroatia, Zdravko Logarusic ameiongoza Simba kwa mechi ya pili na kushinda zote.
Hivi karibuni aliiongoza klabu yake katika mchezo wake wa kwanza wa kirafiki dhidi ya KMKM Ya Zanzibar na kuibuka na ushindi wa mabao 2-1.
Kikosi cha Yanga leo: Juma Kaseja, Mbuyu Twite, David Luhende, Nadir Haroub ‘Cannavaro’, Kevin Yondan, Athumani Iddi ‘Chuji’, Haruna Niyonzima, Frank Domayo, Didier Kavumbangu, Mrisho Ngassa na Hamisi Kiiza.
Wachezaji wa Akiba: Deo Munishi ‘Dida’, Oscar Joshua, Juma Abdul, Simon Msuva, Rajab Zahir, Hassan Dilunga, Emmanuel Okwi, Jerry Tegete, Relliant Lusajo, Nizar Khalfan, Hamisi Thabit na Said Bahanuzi.
Kikosi cha Simba SC; Ivo Mapunda, Haruna Shamte, Issa Rashid ‘Baba Ubaya’, Joseph Owino, Donald Mosoti, Jonas Mkude, Haroun Chanongo, Henry Joseph, Amisi Tambwe, Said Ndemla na Awadh Juma. 
Wachezaji wa akiba: Yaw Berko, Omary Salum, William Lucian ‘Gallas’, Ramadhan Chombo ‘Redondo’, Ramadhani Singano ‘Messi’, Zahor Pazi na Amri Kiemba.

0 comments:

 
https://www.sexmutant.com/ https://www.sexindrag.com/ porn movies sex videos hd porno video