Na Baraka Mpenja kwa msaada wa Sportsmail
Tel: 0712461976 au 0764302956
Cristiano Ronaldo ameifungia bao Real Madrid jana usiku na kuvunja rekodi ya mmoja wa washambuliaji waliopo katika orodha ya kufunga mabao mengi zaidi enzi zao wakisakata soka.
Mshambuliaji huyo raia wa Ureno amefunga mabao 164 katika michezo 151 na kuvunja rekodi ya mshambuliaji wa zamani wa Mexico, Hugo Sanchez aliyefunga mabao 164 katika mechi 207.
Ronaldo ameingia katika orodha ya wafungaji wanne wa juu waliowahi kufunga mabao mengi katika historia ya Real, lakini amebakiwa na rekodi tatu kuzivunja, yaani ya Santillana mwenye magoli 186, Alfredo Di Stefano magoli 216 na Raul aliyetia kambani magoli 228.
Real Madrid waliwafunga Valencia mabao 3-2 jana, shukurani zimwendee Ronaldo kwa kichwa chake mahiri dakika ya 40 kufuatia mpira mzuri wa adhabu uliochongwa na Agel Di Maria alimbadili Gareth Bale katika mchezo huo.
Madrid walipata bao la tatu na la ushindi kupitia kwa kinda wao mwenye miaka 20 Jese Rodriguez katika dakika ya 84.
Bao la kwanza lilifungwa na Angel Di Maria katika dakika ya 28 kufuatia kuwazidi ujanja mabeki wa Valencia.
Mabao ya Valencia yalifungwa na Pablo Piatti dakika ya 34 na Jérémy Mathieu dakika ya 62.
Kikosi cha Valencia jana: Guita, Pereira, Ruiz, Mathieu, Romeu, Feghouli, Bernat, Parejo (Banega, 84), Cartabia, Piatti (Guardado, 80), Jonas.
Kikosi cha Real Madrid: Lopez, Arbeloa (Carvajal, 80), Ramos, Nacho, Marcelo, Alonso, Modric, Di Maria (Illarramendi, 87), Isco (Jese, 73), Ronaldo, Benzema.









0 comments:
Post a Comment