Monday, November 4, 2013

17
Kocha wa Yanga, Ernie Brandts (Kushoto) wakiwa na msaidizi wake, Fredy Ferlix Minziro (Kulia)
Na Braaka Mpenja wa Fullshangwe, Dar es salaam
MABINGWA watetezi wa ligi kuu soka Tanzania bara, Dar Young Africans wamebeza watani zao wa jadi , Wekundu wa msimbazi Simba Sc kwa mwendo wao wa kusuasua na kuwatoa katika Kinyang`anyiro cha ubingwa msimu huu.
Kocha msaidizi wa Yanga, Fredy Ferlix Minziro, Catalaiya Majeshi baba Isaya, amesema mbio za ubingwa ni baina yao na Azam kwani Simba wameshajitoa kwani kikosi chao kina matatizo mengi, na kwa upande wa Mbeya City amesisitiza kuwa hawana uwezo wa kupambana mpaka mwisho, hivyo  mzunguko wa pili watalegeza kamba na kuwa timu ya kawaida sana.
“Ligi ni ya kawaida sana ingawa kuna ushindani kiasi fulani, msimu uliopita tulimaliza mzunguko wa kwanza tukiwa na pointi 29 na msimu huu tutamaliza tukiwa nazo 28. Katika mbio za ubingwa Simba wameshajitoa, kwahiyo timu zinazowania ni Yanga na Azam, na si timu yoyote”. Alisema Minziro.
Minziro alisema mzunguko wa pili Mbeya City watalegea kwani watakutana na vijana wenzao ambao sasa wataingia uwanjani kwa kushindana nao na kuondoa mawazo kuwa ni timu ndogo iliyopanda ligi kuu.
“Mbeya City imepanda daraja juzi juzi tu, kila timu ilipokuwa inakutana nayo ilikuwa inachukulia kama timu ndogo tofauti na timu za Simba na Yanga, Mzunguko wa pili watakumbana na changamoto kubwa na lazima wawaache Yanga na Azam fc katika mbio za ubingwa”. Aliongeza Minziro.
Kocha huyo na mchezaji wa zamani wa Yanga, aliongeza kuwa timu ndogo zinapokutana na timu kubwa huwa zinatoa macho yao kwa nguvu zote, lakini zikikutana zenyewe huwa zinacheza soka la kawaida.
Akizungumzia mchezo wa kufunga pazia la mzunguko wa kwanza wa ligi kuu bara dhidi ya JKT Oljoro uwanja wa Taifa Alhamisi (Novemba 7 mwaka huu), Minziro alisema kikosi kinaendelea vizuri, wachezaji wote wapo katika morali kubwa na wanajiandaa kuwainua vitini mashabiki wao watakaofurika dimbani.
“Ninachowaambia wana Yanga ni kuwa pamoja na kiwasapoti wachezaji wao, kuna wana Yanga wachache ambao wanafanya mambo ambayo si ya kimpira, mara wanawazomea wachezaji wao, waache mara moja tabia hii”. Alisema Minziro.
Yanga kwa sasa wapo nafasi ya tatu wakiwa na pointi zao 25, wakati Mtani wao Simba yupo nafasi ya nne na pointi 21, na katika nafasi ya kwanza Azam fc wanabarizi wakiwa na pointi 26 sawa na Mbeya City waliopo nafasi ya pili lakini wanazidiwa wastani wa mabao ya kufunga na kufungwa.

0 comments:

 
https://www.sexmutant.com/ https://www.sexindrag.com/ porn movies sex videos hd porno video