Monday, November 4, 2013

Na Baraka Mpenja , Dar es salaam
VINARA wa ligi kuu soka Tanzania bara, klabu ya Azam fc wana `Lambalamba` wamekiri kukabiliwa na mchezo mgumu zaidi dhidi ya Mbeya City siku ya alhamisi (Novemba 7 mwaka huu) uwanja wa Azam complex, Chamazi, Nje kidogo ya Dar es salaam.
Afisa habari wa klabu hiyo, Jafary Idd Maganga amesema katika ligi hakuna mechi nyepesi na hiyo ndiyo falsafa yao, lakini mchezo ujao dhidi ya timu wanayofukuzana nayo ni mgumu zaidi kwani vijana hao ni hatari na wanashindana mwanzo mwisho.
“Tulianza ligi kwa sare nyingi, watu walitudharau na kusema hatuna lolote, sasa ni mechi tano tumeshinda mfululizo na tupo kileleni. Lengo letu ni kuendelea kushikilia usukani, hivyo tunajiandaa kwa nguvu zote kuhakikisha tunapata ushindi mbele ya Mbeya City, vijana machachari kabisa”. Alisema Jafary.
TFF Azam FC 
Jafary aliongeza kuwa vijana wao akiwemo Farid Musa, Joseph Kimwaga wamekuwa wakisaidiwa na wachezaji wakubwa kupata uzoefu na wataendelea kufanya hivyo kwani Azam fc ni timu pekee hapa Tanzania iliyoanzishwa na kujenga kituo cha kulelea vijana kwa wakati huo huo.
“Azam fc ni timu inayoamini soka la vijana, tunajua kuwa vijana hawawezi kuwa tegemeo, sisi tuna wachezaji wazoefu ambao wanafanya kazi ya kuwaongoza vijana wetu. Kocha wetu pia amekubali mfumo wetu na tutaendelea hivi mpaka mwisho”. Alisema Jafary.
1239581_432061306914560_864943343_n 
Kwa upande wao Mbeya City kupitia kwa kocha wao mkuu, Juma Mwambusi wametamba kupambana vikali na Azam fc ambao ni timu bora ili kuvuna pointi tatu muhimu kwao.
Mwambusi alisema maandalizi waliyoyafanya kutoka awali ni kwa mechi zote 26 za ligi kuu soka Tanzania bara, ingawa wanatambua ugumu wa Azam, lakini wamejiandaa kutafuta ushindi ili kushika usukani kwa mara ya kwanza tangu kuanza kwa ligi.
“Kwanza niwapongeze vijana wangu kwa kuendelea kufuata maelekezo yangu, wanacheza vizuri na ndio maana najiamini ninapoenda kukutana na Azam fc wakiwa nyumbani. Niwaombe mashabiki wa soka Mbeya, waje kwa wingi kuishangilia timu yao kwani ipo tayari kwa mapambano”. Alisema Mwambusi.

0 comments:

 
https://www.sexmutant.com/ https://www.sexindrag.com/ porn movies sex videos hd porno video