Sunday, November 3, 2013


016
Rais wa TFF, Jamal Malinzi jana alikabidhiwa rasmi ofisi na Rais aliyemaliza muda wake, Leodigar Chila Tenga
Na Baraka Mpenja , Dar es salaam
 BAADA ya Rais wa zamani wa shirikisho la soka Tanzania, TFF Leodigar Chila Tenga kukabidhi ofisi hapo jana kwa Rais Mpya, Wadau wa soka nchini Tanzania hususani wanaopenda maendeleo wametakiwa kumuunga mkono Rais wa sasa wa TFF, Jamal Emily Malinzi ili kufanikisha ilani yake iliyosheheni mipango mingi yenye tija kwa mpira wa Tanzania.
Mshambuliaji wa zamani wa klabu ya Yanga na Taifa Stars, Sekloja Johnson Chambua ambaye kwa sasa ni kocha wa mpira wa miguu amesema Rais Malinzi ana sera nzuri za kuendeleza soka la Tanzania, lakini peke yake hataweza kufikia malengo yake, hivyo wadau wampe sapoti kubwa ili taratibu zake alizojipangia ziweze kufikiwa.
“Malinzi ameongelea vizuri mipango yake ya kuendeleza soka la vijana, sera alizosema ni nzuri, kinachofuata ni utekelezaji wa sera zake. Mara nyingi tumekuwa tukizungumza sana bila kutekeleza, cha msingi kwa Rais wetu ni kutekeleza kila alichosema, lakini bado wadau nao wanatakiwa kuwa karibu naye”. Alisema Chambua.
Chambua alisema soka la vijana ndio msingi muhimu, hivyo lazima wapenda michezo kuungana kutekeleza sera zake, ila ni muhimu kwa Malinzi kuhakikisha suala la makocha linawekewa uzito kama alivyoahidi.
“Kuna makocha wengi wenye kozi za awali hapa nchini, nimuombe Rais Malinzi kuwasaidia makocha hawa kujiendeleza ili wawe bora zaidi. Kama unavyojua nchi hii ni kubwa, tunatakiwa kusambaza makocha kila sehemu ili kuibua na kuendelea vipaji kwa vijana”. Alishauri Chambua.
Kwa upande wake Mkurugenzi wa kituo cha vijana cha Morogoro (Morogoro Youth Soccer Academy), Rajab Kindagule amesema walikuwa na ushirikiano mkubwa na uongozi wa Tenga, hivyo wanasubiri ushirikiano kama huo au zaidi kutoka kwa Rais mpya , Jamal Malinzi.
“Sijui Malinzi anataka mfumo gani, lakini ameongea vizuri katika sera zake, inaonekana ana nia ya kuendeleza soka la vijana. Tunapanga kuonana naye ili tumpe pongezi na kumueleza mambo mbalimbali yahusuyo soka”. Alisema Kindagule.
Kindagule aliyewaibua wachezaji maarufu na vijana kwa sasa, Shomary Kapombe aliyeko Ufaransa, Willium Lucian `Gallas` , Edward Christopher waliopo Simba na wengine wengi aliongeza kuwa ni lazima Malinzi apewe sapoti kubwa kwani kiukweli ilani yake imezungumzia mambo mengi ya msingi katika soka la Tanzania.
Naye kocha wa klabu ya Njombe mji na mjumbe wa kamati ya ufundi ya klabu ya Simba sc, John William `Del Piero` amemuomba Rais Malinzi kukaa chini na kamati yake ya utendaji na kujenga ushirikiano mkubwa ili kufanikisha ilani yake inayoonekana ngumu kulingana na uzito wa mambo aliyoyasema.
Rais Malinzi ameweka wazi sera zake na kiukweli kagusa maeneo mengi yenye mapungufu, lakini tukimuacha afanye peke yake na kuendekeza makundi na tofauti za kiushabiki, basi atashindwa kufanikisha mengi.
“Binafsi nina imani kubwa na Bwana Malinzi, ni mtu wa mpira, ana uzoefu mkubwa. Nadhani atashirikiana na viongozi wenzake kufikia malengo”. Alisema Piero.
Leodgar-Tenga
Rais wa TFF aliyemaliza muda wake, Leodigar Tenga
Jana wakati anakabidhiwa ofisi, Rais Malinzi alisema  Uongozi wake unakabiliwa na nyingi ambazo hawezi kuzitaja kwa pamoja, lakini chache zinazohitaji ufumbuzi wa haraka ni:
Hii ni sehemu ya Hotuba ya Malinzi jana, soma ili utambua nini alichosema:
Mashindano yanayotukabili.
Malinzi alisema ; “Tunakabiliwa na mashindano mbalimbali ya kimataifa. Mfano ni mechi ya marudiano ya U/20 wanawake dhidi ya Msumbiji wiki ijayo, Mitoano ya mashindano ya Afrika wanawake mapema mwakani, Mashindano ya Chalenji Novemba mwaka huu, na mashindano ya kufuzu AFCON 2015. Yote haya yanahitaji maandalizi ya haraka”. 
Programu ya vijana.
“Ilani yangu ya uchaguzi ilielezea azma ya Tanzania kuomba uenyeji wa fainali za vijana za Afrika U/17 mwaka 2019. Jambo hili tutalizungumzia kwenye kikao chetu cha utendaji leo. Ili tuwe na timu nzuri ya kucheza fainali hizo tukiwa wenyeji hatuna budi mwaka kesho kuunda timu ya Taifa ya U/12 itakayokua pamoja kuelekea 2019. Programu yetu ya vijana tutakayoiandaa sharti  ijielekeze kwenye ratiba hii.”
Udhamini wa timu za vijana na za wanawake
“Hii ni changamoto kubwa sana kwa TFF. Timu zetu za Taifa kuanzia zile za wakubwa hadi za vijana ni brands, na kama ni brands inabidi ziingizwe sokoni, ziuzwe kwa tunaodhamiria wawe wadhamini wa hizo timu. Kitengo cha masoko lazima kiimarishwe ili kukabiliana na changamoto hizi. Mdhamini ni mfanyabiashara, anapotoa pesa kudhamini brand fulani anategemea matokeo mazuri kwake kwa njia ya kukuza biashara zake. Twende kwa wadhamini tuwashawishi waone watafaidikia nini (leverage) kwa kudhamini timu zetu. Tusisubiri waje tuwafuate sisi.”
Uwekezaji
“Jitihada za haraka lazima zifanyike kuiongezea TFF uwezo wa kiuchumi. Ni muhimu mtaalam mshauri (consultant) atafutwe atufanyie mchanganuo wa uwekezaji katika ardhi yetu hii ya Karume ili tuwekeze kitega uchumi kama ilivyokubaliwa kwenye mkutano mkuu. Aidha bidhaa zenye nembo yetu zianze kuuzwa kwa utaratibu maalum ili shirikisho lipate haki yake.”
“Kabla sijamaliza kuzungumza, niongelee suala la fujo viwanjani. Mpira ni dakika tisini. Katika kipindi hicho uamuzi wa mwamuzi unakuwa ni wa mwisho. Tusifiche upungufu wa timu zetu kwa kujificha nyuma ya kivuli cha mwamuzi. Waamuzi wakionekana wamefanya makosa yawe ya makusudi au ya bahati mbaya vyombo vya kuwahukumu vipo, mahakama ya waamuzi sio mashabiki. Kitendo cha mashabiki kufanya fujo kabla, wakati na baada ya mechi ya mpira kamwe hakikubaliki mahali popote duniani.  Kanuni za FIFA, CAF na TFF ziko wazi na adhabu zinajulikana. Moja ya adhabu hizi ni timu husika kucheza kwenye uwanja mtupu usio na mashabiki kama ilivyowatokea Al Ahly na Zamalek huko Misri au kucheza nje ya uwanja wako kama ilivyowatokea Senegal ambao baada ya vurugu Dakar, Senegal waliamriwa na FIFA mechi zao za nyumbani wachezee nje ya nchi na wakachagua kuchezea Morocco.”
“Ndugu zangu yaliyotokea majuzi Mbeya na Dar es salaam wote tumeyasikia na wengine miongoni mwetu hapa ni mashuhuda. Ninasema iwe mara ya kwanza na y a mwisho. Kwenye masuala ya kutekeleza mahitaji ya kanuni uongozi wangu hautaionea haya klabu yoyote, iwe mpya au kongwe kwenye ligi yetu. Ni jukumu la viongozi wa klabu kudhibiti wanachama na wapenzi wao. Tabia ya benchi la ufundi kutoa matamshi yanayoweza kuamsha hisia za mashabiki ni kinyume na taratibu na kanuni ziko wazi kuhusu jambo hili. Viongozi wa klabu na mabenchi yao ya ufundi wakishindwa kutekeleza wajibu wao tusilaumiane.”
“Ndugu zangu ya kufanya ni mengi katika kuiendeleza soka yetu. Tunashukuru Mungu kuwa uwezo wa kukabiliana na changamoto hizi tunao na tuna ari na nia ya kusukuma mbele gurudumu la maendeleo ya mpira. Ombi langu kwenu nyote ninaomba ushirikiano wa wadau wote kuanzia Serikali, Halmashauri, mashirika ya umma na binafsi na NGO’s, nina imani tukishikamana tutaifikia ndoto yetu ya kuing’arisha Tanzania kimpira kwenye anga za dunia.”

0 comments:

 
https://www.sexmutant.com/ https://www.sexindrag.com/ porn movies sex videos hd porno video