KLABU
 ya Manchester United imepata pigo kubwa baada ya nyota wa Barcelona 
iliyekuwa inamtaka, Andres Iniesta kukubali kusaini Mkataba mpya na 
klabu yake hiyo ya Hispania.
Mkurugenzi
 wa Michezo wa Barca, Andoni Zubizarreta amesema kiungo huyo yuko karibu
 kusaini Mkataba mpya na vinara hao wa La Liga.
Mchezaji
 huyo mwenye umri wa miaka 29 ilielezwa hafurahii maisha Nou Camp 
kutokana na kutofautiana na mabosi wa timu hiyo, hivyo kumpa matumaini 
kocha David Moyes, ambaye amekuwa akimmezea mate na kutaka kumsajili 
Januari. 
Pamoja na hayo, kipa wa zamani wa Barca, Zubizarreta amepuuza madai kwamba Iniesta ataihama klabu hiyo.
Anabaki? Andres Iniesta ilielezwa hafurahii maisha Barcelona, lakini sasa imeelezwa atasaini Mkataba mpya 

Pigo: Kocha wa Manchester United, David Moyes (juu) ilielezwa anataka kumsajili Iniesta Januari





0 comments:
Post a Comment