Monday, November 11, 2013


DSC_1625 
Na Baraka Mpenja , Dar es salaam
KIUNGO mahiri, mtaalamu wa kupiga pasi na kumiliki gozi akiwa dimbani wa Mabingwa watetezi wa ligi kuu soka Tanzania bara na kikosi cha timu ya Taifa, `Taifa Stars`, Frank Domayo amewataka vijana wenzake wanaopewa nafasi na makocha wao kucheza mechi mbalimbali kuonesha juhudi kubwa na kuzitendea haki nafasi hizo.

Domayo ameuambia mtandao wa MATUKIO DUNIANI kuwa ligi imekuwa tamu sana kutokana na timu nyingi kuwapa nafasi vijana ambao wana malengo ya kutafuta maisha na ndio maana wakiingia uwanjani wanataka kuonekana zaidi , hivyo kupelekea mechi kuwa ngumu.

“Mimi nafurahi sana kuona vijana wanapewa nafasi, kiukweli wana viwango vya hali ya juu. Tumemaliza mzunguko wa kwanza tukiwa nafasi ya kwanza, lakini ligi ni ngumu sana, vijana wana kasi kubwa na wanapamabana sana”. Alisema Domayo.

Domayo alisema soka la sasa linahitaji kujituma zaidi kwani ni ajira, hivyo vijana lazima wajue kuwa mpira wa miguu hauna uchawi, bali ni mazoezi na kujituma.

“Tusilewe sifa, tuzingatie programu za mazoezi za makocha wetu, tujitume na kuwa na utamaduni wa mazoezi binafsi, Kocha mzuri huwa anamtazama mchezaji mazoezini, hivyo vijana wakipewa nafasi ya kuonesha vipaji vyao wahakikishe hawafanyi makosa”. Alishauri Domayo.

Kiungo huyo tegemeo wa Yanga alisema kwasasa wapo mapumzikoni, lakini yeye ana mikakati yake ya kujiweka sawa kwa ajili ya mzunguko wa pili na michuano ya kimataifa mwakani.

“Tuna kazi ngumu ya kutetea ubingwa wetu, pia tunakabiliwa na michuanoi ya Afrika, lazima nijiweke fiti kwa wakati wote kabla ya kuanza mazoezi ya pamoja”. Alisema Domayo.

Kinda huyo amekuwa chaguo la kwanza kwa kocha mkuu wa timu ya Yanga, Ernie Brandts na amekuwa akicheza mechi nyingi sana kutokana na uwezo wake, lakini pia ni kivutio kikubwa kwa kocha wa Taifa Stars, Kim Poulsen.

0 comments:

 
https://www.sexmutant.com/ https://www.sexindrag.com/ porn movies sex videos hd porno video