Friday, September 13, 2013


Na Baraka Mpenja, Mbeya
MZUNGUKO wa tatu wa ligi kuu soka Tanzania bara unatarajiwa kuendelea kushika kasi hapo kesho kwa timu zote 14 kushuka dimbani katika viwanja tofauti nchini.
Wekundu wa Msimbazi Simba watakuwa uwanja wao wa  nyumbani wa Taifa jijini Dar es salaam baada ya mechi mbili za Ugenini dhidi ya wakata miwa wa mashamba ya Manungu Turiani mkoani Morogoro, Mtibwa Sukari.
Mechi hiyo imevuta hisia za mashabiki kutokana na ugumu wa wana TamTam ambao msimu uliopita walivuta sharubu za Simba na kuwatuliaza tuli.
10 
Mabingwa watetezi wa ligi hiyo, klabu ya Yanga ya Dar es salaam kwa mara ya kwanza wanatoka ugenini na kesho wana kibarua kizito mbele ya timu mpya ya Mbeya City ya jijini hapa katika uwanja wa Sokoine.
Kwa upande wa wagosi wa kaya, Coastal Union wamerejea kwao CCM Mkwakwani jijini Tanga na hapo kesho wanawakaribisha wachovu wa ligi hiyo, Tanzania Prisons ambao kwa Sasa wapo mkiani katika msimamo.
Charlse Mkwasa na Ruvu Shooting yake watakuwa katika uwanja wao wa Mabatini mkaoni Pwani kukabiliana na Mgambo JKT, huku tambo zikitawala kwa kila timu kuibuka kidedea katika mchezo huo.
Dimba la Sh. Amri Abeid Kaluta jijini Arusha litahimili daluga za wenyeji JKT Oljoro dhidi ya maafande wenzao kutoka Tabora, Rhino Rangers.
Macho ya mashabiki wengi wa Soko yatakuwa katika mechi za vigogo wa Soka la Tanzania, Simba na Yanga pamoja na Azam fc kwani ni ukweli kuwa timu hizi zinavuta hisia za mashabiki wengi kila kona ya Tanzania. 946002_619805171393176_2049843130_n 
Kwa Mbeya, homa ya pambano la kesho inazidi kupanda huku kila kona hadithi ikiwa ni mechi hiyo ambayo inatarajiwa kushuhudiwa na maelfu ya mashabiki wa soka kwa kiingilio cha Tsh. 5,000/=.
Chama cha soka mkoani Mbeya, MREFA kimesema Maandalizi ya mechi hiyo yamekamilika kuanzia masuala ya uuzaji wa tiketi na ulinzi kwa kushirikiana na jeshi la polisi.

0 comments:

 
https://www.sexmutant.com/ https://www.sexindrag.com/ porn movies sex videos hd porno video