Tuesday, July 2, 2013


mtibwa-sugar-feb02-2013

Na Baraka Mpenja 
Wakata miwa wa mashamba ya miwa ya Manungu Turiani mkoani Morogoro, wana “TamTam “ Mtibwa Sugar wanaofundishwa na kocha mzawa Mecky Mexime wanatarajiwa kuanza kupiga jalamba la uhakika katikati ya mwezi huu wa saba ili kujiandaa na mitanange ya ligi kuu soka Tanzania bara msimu mpya unaotarajiwa kuanza Agosti 24.

Mwenyekiti mwenye dhamana ya kuiongoza timu hiyo kubwa nchini Tanzania yenye historia ya kuzisumbua Simba na Yanga na kutwaa taji miaka ya nyuma, Jamal Baiser amesema kwa sasa wanafanya mipango ya kusajili wachezaji wa kuziba nafasi zilizoachwa wazi  kufuatia baadhi ya wachezaji kutimka klabuni hapo.

“Mpaka sasa hatujasajili wachezaji, lakini mipango yetu ni kusajili wachezaji wapatao watano, na baada ya kukamilisha taratibu zote, tutawajulisha mashabiki wetu. Kikubwa ni kwamba, tunahitaji kuwa na timu nzuri zaidi kuliko misimu mitatu iliyopita”. Alisema Baiser.

Baiser alisema kwa muda mrefu sasa,  Mtibwa sugar haifanyi vizuri sana wala vibaya sana, lakini kwa msimu ujao wanajiandaa kuwa timu bora zaidi,  huku wakichanganya damu changa na kongwe katika kikosi chao.

Mwenyekiti huyo alisema timu yao amepoteza baadhi ya wachezaji akiwemo Issa Rashid “Baba Ubaya” aliyejiunga na wekundu wa Msimbazi Simba pamoja na Hussein Javu anayesemekana kusaini yanga, lakini wana wachezaji wengine wa kuziba nafasi zao na wengine watawasajili.
“Walikuwa wachezaji muhimu sana, lakini hatuna jinsi, soka ni ajira yao, hatuna uwezo wa kuwabania nafasi ya kucheza klabu  nyingine, ila kiuhakika tunao wachezaji wengi sana wa kuziba nafasi zao nab ado tunatafuta nyota wengine wa kuwasainisha”. Alisema Baiser.

Akizungumzia suala la Javu kusaini Yanga, Baiser alisema Mtibwa Sugar  ilikuwa na mkataba naye, lakini Yanga waliomba ruhusa ya kuzungumza naye na wao wakakubali.

“Walituomba kuongea na Javu, tuliwaruhusu. Kama wamekubaliana na kumpa mkataba sisi bado hatuna taarifa ofisini, Yanga bado hawajaja kufanya taratibu za uhamishoi, kwahiyo hatujui kama wameshamalizana naye, hivyo sitaki kulizungumzia sana kwa sasa, wakati utafika nitazungumza”. Alisema Baiser.

Baiser alisema Javu alikuwa mchezaji muhimu sana, lakini wanajipanga kutafuta mbadala wake.

0 comments:

 
https://www.sexmutant.com/ https://www.sexindrag.com/ porn movies sex videos hd porno video