Tuesday, July 2, 2013

msondp 
Na Baraka Mpenja
Timu za netiboli za Jeshi la Polisi na Halmashauri ya jiji, mkoani Mbeya zinatarajia kuanza mazoezi ya mapema ili kufanya vizuri katika michuano ya ligi kuu daraja la kwanza ya mchezo wa mpira wa pete inayotarajiwa kufanyika kwa mara ya pili mfululuzo jijini Mbeya kuanzia Agosti 24 hadi septemba 7 mwaka huu.
Akizungumza kwa njia ya simu kutoka jijini Mbeya, mwenyekiti mwenye dhamana ya kuongoza mchezo wa netiboli jijini humo, Mary Mng`ong`o ameipasha MATUKIO DUNIANI kuwa hakutakuwepo na ongezeko la timu za mkoa huo, lakini wanahakikisha timu wakilishi zinaanza maandalizi mapema.
“Tumelazimika kuandaa michuano hii mikubwa ya kitaifa kwa mara nyingine, hatuna jinsi kwani aliyekuwa mgeni rasmi mwaka jana, Naibu waziri wa Elimu na Mafunzo ya ufundi, Mhe. Philp Mulugo alikitaka chama chetu kuandaa tena kwa ufanasi zaidi. Tulikubali na sasa maandalizi yameshaanza”. Alisema Mng`ong`o.
Kiongozi huyo alisema Uongozi wa chama cha mkoa tayari umeshaziandikia klabu zao barua ya kuanza maandalizi, huku wakiziomba kuandika barua na kutuma CHANETA ili kuthibitisha ushiriki wao.
Mng`ong`o alisema mwaka jana walikumbana na ukata mkubwa sana kuendesha mashindano hayo, hivyo anawaomba wadau kujitokeza kwa wakati huu mgumu kwao ili kuchangia na kufanikisha michuano hiyo kwa kiwango kukubwa zaidi ya mwaka jana.
“Ndo kwanza tunaanza kujipanga, wadau wana nafasi kubwa sana. Ni muhimu sana kuchangia kwa moyo, kwani wakifanya hivyo basi kila kitu kitaenda sawa”. Alisema Mng`ong`o.
Mwenyekiti huyo alisema tayari taarifa imeshatolewa kutoka CHANETA kuwa Agosti 24 yataanza kutimua vumbi, na tayari uongozi wa chama hicho chini ya mwenyekiti wake Anna Faith Kibira amesharidhia mkoa huo kuwa mwenyeji wa michuano hiyo.

0 comments:

 
https://www.sexmutant.com/ https://www.sexindrag.com/ porn movies sex videos hd porno video