Tuesday, July 2, 2013

DSCN0379 
Kocha wa Mbeya City, Juma Mwambusi (waliokaa wapili kutoka kulia). picha kwa hisani ya Malafayaleleo.blogspot.com

Na Baraka Mpenja 
WAKATI Timu mbalimbali ligi kuu soka Tanzania bara zikianza maandalizi makali ya msimu mpya wa ligi kuu  unaotarajiwa kuanza kutimua vumbi Agosti 24 mwaka huu, nao wakali wapya wa ligi hiyo Mbeya City ya jijini Mbeya wameanza kujifua chini ya kocha wao mkuu Juma Mwambusi.
Akizungumza na mtandao wa MATUKIO DUNIANI kocha mkuu wa klabu hiyo Juma Mwambusi, amesema wachezaji kutoka mikoani wameanza kuwasili kuanzia jana, huku akieleza kuwa anajipanga kuongeza wachezaji wachache katika kikosi chake alichotoka nacho  ligi daraja la kwanza msimu uliopita.
“Wachezaji wengi ni walewale, nina mpango wa kuongeza nyota wachache, wengi nitawapandisha kutoka kikosi B, lakini wachezaji wengi waliopandisha timu ligi kuu nimewaacha ila kuna nafasi chache nitaziba hivi karibuni”. Alisema Mwambusi.
Mwambusi alisema katika kikosi chake hana tabia ya kuwapa majina wachezaji kwa kuwapa uhakika wa namba, kwani falsafa yake ni kuchezesha wachezaji wote bila kujali majina yao.
“Mimi siku zote falasafa yangu ni ileile, wachezaji wote wanaong`ara wameweza kupata nafasi hiyo kwa sababu walipewa nafasi ya kucheza, hivyo nitawapa wachezaji wote nafasi ya kucheza ili waongeze uzoefu”. Alisisitiza Mwambusi.
Kuhusu kusajili wachezaji wenye uzoefu mkubwa na mikikimikiki ya ligi kuu, Mwambusi alisema hana mpango wa kusajili wakongwe kutokana na kikosi chake kuwa na vijana wengi ambao wanafanya vizuri.
“Mbeya City ina kikosi bora cha vijana, ninavyozungumza hapa kipo mkoani Iringa wilaya ya Mufindi kushiriki michuano ya kombe la Muungano Mufindi, ni kikosi kizuri sana, kinaongozwa na kocha wangu msaidizi Maka Mwalwisyi ambaye anafanya kazi nzuri. Ni matumaini yangu hawa vijana ni msingi mkubwa wa klabu yangu na watapewa nafasi”. Aliongeza Mwambusi.
Mwambusi alisema kikosi chake kinahitaji kujifua kwa nguvu kuhimili mitanannge ya ligi kuu, kwani ligi ya Tanzania bara imekuwa na ushindani mkubwa sana.
“Ligi imebadilika sana, niliifundisha Prisons miaka ya nyuma, sasa naona mambo yamebadilika sana, lakini nina uhakika kwa uzoefu wangu nitajipanga vizuri na kupambana hadi mwisho”. Alisema Mwambusi.
Mbeya City ni miongoni mwa timu tatu zilizopanda ligi kuu soka Tanzania bara msimu ujao, wakati nyingine ni Maafande wa Rhino Rangers ya Tabora, na Ashanti United ya Dar es salaam.
Msimu uliopita timu tatu za Africa Lyon ya Dar es salaam, Toto Africans ya Mwanza na Polisi Morogoro zilishuka daraja na sasa zinaendelea na mazoezi ya kujiandaa na msimu mpya wa ligi daraja la kwanza.

0 comments:

 
https://www.sexmutant.com/ https://www.sexindrag.com/ porn movies sex videos hd porno video