Tuesday, July 2, 2013


Na Baraka Mpenja
KIUNGO nyota wa klabu ya Simba, Wekundu wa Msimbazi “Taifa Kubwa” Ramadhan Chombo “Redondo” wa Kitanzania mwenye mbwembwe na sifa kubwa ya kupaka gozi rangi akiwa uwanjani, amesema hatima yake ya kuichezea klabu ya hiyo msimu ujao itajulikana jumatatu ya wiki ijayo ambapo atakutana na viongozi kuzungumzia suala lake.

Redondo amezungumza na MATUKIO DUNIANI na kuweka wazi kuwa bado ni mchezaji wa Simba kwani ana mkataba nao.

“Mimi nina mkataba na Simba, mpaka sasa hatujazungumza lolote kuhusu hatima yangu. Wiki ijao siku ya jumatatu kila kitu kitakuwa wazi ambapo nitakutana na uongozi wa klabu yangu”. Alisema Redondo.

Kiungo huyo mwenye uwezo wa aina yake aliongeza kuwa bado anahitaji kucheza soka na kuitumikia klabu ya Simba licha ya kusimamishwa msimu uliopita na aliyekuwa kocha wa klabu hiyo, Mfaransa Patrick Liewig kwa tuhuma za utovu wa nidhamu.

“Tangu msimu umeisha sijazungumza na viongozi wangu, bado nina nia ya kuichezea klabu yangu. Mpira ni kazi yangu na naiheshimu sana”. Alisema Redondo.

Redondo hakusita kuweka wazi kuwa yuko tayari kusakata kandanda klabu yoyote ya Tanzania endapo itafuatwa na kufanya mazungumzo yenye maslahi.

“Kama sitapata nafasi ya kucheza Simba, naweza kujiunga na klabu yoyote ile ya hapa nyumbani au nje ya nchi. Kikubwa ni maslahi kwani soka ndio kazi yangu rasmi”. Alisema Redondo.

Nyota huyo aliyeichezea Azam fc msimu wa 2011/2012 akitokea Simba na msimu wa 2012/2013 kurudi kwa wekundu wa Msimbazi Simba alisisitiza kuwa kwa sasa anaendelea na mazoezi ya kujiweka sawa kwani anatambua kuwa soka halina uchawi, bali ni mazoezi na kutambua wajibu wake.

“Kwasasa naendelea na mazoezi binafsi, nasubiri hatima yangu Simba, nasisitiza, nina mkataba na Simba, jumatatu nitasema nini hatima yangu”. Alisema Redondo.

Chombo ni miongoni mwa wachezaji waliokalia kuti la moto enzi za kocha Mfaransa Patrick Liewig ambaye kwa sasa amefungashiwa virago na kumuachia kocha mzawa Abdallah Kibadeni “King Mputa”.

Chombo alituhumiwa na Liewig kuwa ni mtovu wa nidhamu, hivyo yeye na wenzake akina Abdallah Juma, Ferlix Sunzu, Mwinyi Kazimoto, Paul Ngalema, Amir Maftah, Haruna Moshi “Boban”, Juma Nyoso walisimamishwa na kocha Liewig. 

Miongoni mwa wachezaji hao, Mwinyi Kazimoto pekee ndiye aliyesajiliwa, huku Ferlix Sunzu mkataba wake akimalizika, wakati wengine wametupiwa virago.

0 comments:

 
https://www.sexmutant.com/ https://www.sexindrag.com/ porn movies sex videos hd porno video